VETA YAJA NA KONA YA WATOTO SABASABA

Chuo Cha Mafunzo na Ufundi Stadi VETA) Songea imekuja na kona ya watoto katika maonesho ya 49 ya kimataifa ya biashara yanayoendelea kwa lengo la kuibua vipaji na kuwafundisha misingi ya maisha. Faulata Mutalemwa ambaye ni Mwalimu kutoa VETA Songea amesema kupitia kona hiyo ya watoto wanajifunza vitu mbalimbali ikiwemo stadi za mikono mbalimbali na kuondoka nazo.
Akitaja stadi hizo amesema ni pamoja na ushonaji, urembo pamoja na masuala ya umeme. "Kupitia kona ya watoto mtoto anaweza kujifunza vitu mbalimbali vya namna ya kuchana nywele, kutunza ngozi yake, namna ya kushona nguo zake pamoja na kudhiifadhi"amesema Mutalemwa.
Kwa upande wa eneo la umeme amesema mtoto anajifunza namna ya gani taa inawaka huku akifuata hatua nyepesi. Aidha ametoa wito kwa wazazi, walezj kutembelea katika Banda la Veta ili watoto wao waweze kujifunza vitu mbalimbali vinavyohusu maisha.

Comments

Popular posts from this blog

MATAIFA 8 KUIMBA TAMASHA LA PASAKA

PIMEA USIKU WA WANA NDOA ULIVYOFANA MSIFICHANE NA KUWEKEANA VITU

UONGOZI DHAIFU VYATAJWA KUVURUGA TAASISI ZA VIJANA