Posts

Showing posts from August, 2024

TRC YAOMBA RADHI HITILAFU NYINGINE YA TRENI

Shirika la Reli Tanzania (TRC)  imewaomba radhi abiria waliosafiri na treni ya kawaida  kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam Agosti Mosi,2024  kwa kuchelewa kuwasili kutokana na hitilafu ya kiufundi iliyotokea. Treni hiyo iliondoka Dodoma majira ya saa 2:15 usiku   na kupata hitilafu  katika  eneo la Mtaa wa Mshikanano, Kata ya Kihonda Mkoani Morogoro. Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano ,Jamila Mbarouk ilieleza kuwa hitilafu za kiufundi zilitokea majira ya saa 4:33 usiku nakushughulikiwa  kwa muda wa takribani saa moja na kusababisha treni  hiyo ya abiria kutoka Dodoma kuchelewa kuwasili Dar Es Salaam kwa wakati uliopangwa.  Aidha Shirika lilisema kuwa tremi iliyobeba viongozi na wananchi wengine  walitoka Dodoma saa moja usiku baada ya kushiriki sherehe za uzinduzi wa SGR waliwasili Dar es Salaam kwa muda uliopangwa bila hitilafu yoyote.  “TRC inazingatia usalama wa abiria kabla na wakati wa safari ili kuepusha ...

TCRA CCC NA FC WAINGIA MAKUBALIANO KULINDA wATUMIAJI WA MAWASILIANO

Image
  Asasi za kiraia (FCS) na Baraza la ushauri la watumiaji wa huduma za Mawasiliano (TCRA CCC) wameingia Ubia wa miaka mitatu  kushirikiana kulinda haki za watumiaji wa huduma za mawasiliani Tanzania wenye lengo la kuhakikisha haki na uwajibikaji katika kutoa huduma kwa watumiaji na kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi  wanaponunua na kutumia bidhaa. Ubia huo unachangia maendeleo ya masoko na ukuaji wa biashara zinazoheshimu sera za kulinda watumiaji na kuwapa wateja kipaumbele kujijengea hadhi na kuziweka nafasi nzuri kiushindani. Hayo ameyasema Justice Rutenge Mkurugenzi wa Asasi na kiraia (FCS) wakati wakisaini Ubia huo Agosti 6,2024 Jijini Dar es salaam  Aidha Justice amesema ushirikiano huo ni kielelezo  cha nia thabiti ya kuwawezesha watumiaji wa huduma na bidhaa na kukuza haki zao katika soko likiwa na mlengo wa kujenga mazingira bora katika soko kwa watumiaji na huduma za mawasiliano ili wawe wenye taarifa sahihi na kulinda stahiki zao nchini. Sambamba na h...

TANZANIA U19 YANGARA KRIKETI AFRIKA

Image
TIMU ya taifa ya Tanzania ya Kriketi kwa vijana chini ya umri wa miaka 19 imeanza vyema michuano ya Afrika daraja la pili kufuzu Kombe la Dunia baada ya kuichapa Nigeria kwa mikimbio 128-127. Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Gymkhana Dar es Salaam utofauti wa mikimbio ni moja huku Tanzania ikicheza wiketi nne  na Nigeria 10.  Nahodha wa timu hiyo Laksh Bakrania amesema mchezo ulikuwa mzuri na mgumu ila juhudi zao zimewasaidia kupambana na kushinda. Kesho watacheza na Ghana ambao nao wametoka kushinda mchezo dhidi ya Msumbiji kwa mikimbio 81-80. Michuano hiyo ya Afrika inafanyika kwenye viwanja vya Gymkhana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo imeshirikisha nchi nane ambazo ni Tanznia, Nigeria, Malawi , Msumbiji, Ghana, Botswana, Siera Leone na Rwanda. Tanzania ipo kundi B lenye timu za Nigeria, Msumbiji na Ghana huku kundi A kukiwa na Sierra Leone, Rwanda, Botswana na Malawi. Mratibu wa mashindano hayo Atif Salum amesema nchi mbili kwa kila kundi zitaenda kuchez...

MASHINDANO YA CRICKET WORLD CUP AFRICAN

Image
Mashindano ya Cricket World Cup Africa Division 2 Qualifier kuanza kufanyika leo katika viwanja vya Gymkhana Posta jijini Dar es Salaam yakishirikisha nchini nane. Akizungumza na Mratibu wa mashindano hayo, Mratibu wa  CMashindano ya Kriketi Tanzania (TCA), Atif Salim amesema katika michuano hiyo Kuna timu nane na timu zimepangwa katika makundi mawili yenye kila kundi timu nne, "Tanzania ipo kundi  A na Nigeria, Msumbiji na Malawi, huku kundi B likiundwa na Ghana, Botswana, Sierra Leone na Rwanda. "Washindi wawili wa kila kundi watacheza nusu fainali, kisha fainali  na kutafuta mshindi wa tatu.Watakaocheza fainali tayari wote watakuwa wamefuzu kwenda Division I, na nchi itakayokuwa mshindi wa tatu nayo itafuzu kwenda mbele Division I,” amesema Atif. Kwa upande wake Kocha wa timu ya kriketi ya Msumbiji, Filipe Cossa amesema  Tanzania ni ndiyo   timu  inayoweza kumzuia katika mashindano kriketi ya kufuzu kombe la dunia, daraja la pili (Divisheni II) kwa ...