Posts

Showing posts from January, 2026

WANAMITINDO WAPATIWA ELIMU YA FEDHA CRDB BENKI KUINUA BIASHARA NA KUTOA AJIRA

Image
Washonaji Wapatiwa Semina ya Elimu ya Fedha Kuinua Biashara na Kutoa Ajira Washonaji na wabunifu wa mitindo nchini wamepatiwa semina ya elimu ya fedha yenye lengo la kuwawezesha kukuza biashara zao, kutoa ajira kwa vijana na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Jafari Hassanali, amesema tasnia ya mitindo ipo katika safari ya kutoka kwenye kipaji cha kawaida na kuelekea kuwa biashara endelevu yenye mchango mkubwa katika uchumi wa taifa. Amesema ubunifu ulio sambamba na maarifa ya biashara na usimamizi wa fedha ni msingi muhimu wa kushikilia na kuimarisha uchumi wa nchi, akibainisha kuwa sekta ya ubunifu ni miongoni mwa sekta zinazokua kwa kasi na zenye uwezo mkubwa wa kutoa ajira kwa vijana. Akizungumza katika Jukwaa la Tanzania Fashion Forum, Hassanali amewataka wabunifu kutumia mikopo kama nyenzo ya uwezeshaji wa biashara badala ya kuifanya kuwa mazoea. “Unapokopa lazima uelewe kuwa mkopo ...

WAZIRI JUDITH KAPINGA ATEMBELEA KIWANDA CHA KAMAL GROUP

Image
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ametembelea kiwanda cha Kamal Group kwa lengo la kujionea shughuli za uzalishaji zinazoendelea pamoja na kusikiliza changamoto zinazokikabili kiwanda hicho. Katika ziara hiyo, Waziri Kapinga amesisitiza dhamira ya Serikali ya kuendelea kushirikiana kwa karibu na sekta binafsi ili kuboresha mazingira ya viwanda, kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi wa taifa. Amesema Serikali imepokea changamoto zinazohusu upatikanaji wa umeme na maji ambazo zimekuwa zikikwamisha utekelezaji wa shughuli za uzalishaji kwa ufanisi.  Waziri Kapinga ameahidi kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kupitia taasisi husika, hususa TANESCO na DAWASA, ili kuhakikisha miundombinu rafiki inawekwa kuwezesha viwanda kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. Aidha, Waziri Kapinga amepongeza kiwanda cha Kamal kwa mchango wake katika kukuza ujuzi kwa vijana kupitia ushirikiano na taasisi mbalimbali za mafunzo, hatua inayosaidia kuwaandaa vijana kulingana na mahitaji ya...

BABA WATOTI WA RIHANA ANATAKA WATOTO WENGI

Image
Baba watoto wa mwanamuziki Rihanna, A$AP Rocky anasema wanataka kumfikia mtangazaji Nick Canon kuwa na idadi ya watoto wengi ambaye mpaka sasa ana watoto 12. Rapa huyo A$AP Rocky ameongea hilo baada ya kuulizwa kama wana mpango wa kuongeza watoto wengine na mpenzi wake Rihanna. "Chochote ambacho Mungu amenipa ni kama baraka! Tuna timu nzima ya mpira sasa hivi nina karibia kumfikia Nick Canon". Mpaka sasa Rihanna na A$AP wana watoto watatu RZA Athelston Mayers aliyezaliwa 2022, Riot Rose Mayers 2023 na Rocki Irish Mayers 2023. Vipi wewe na mwenzako mna watoto wangapi? mtaongeza wangapi?

TANZANIA (JKCI) MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA KIMATAIFA WA AFYA YA MOYO

Image
Tanzania kuwa kitovu cha Mkutano Mkubwa wa Kimataifa wa Afya ya Moyo 2026 Na Brighitte DAR ES SALAAM ZAIDI ya watafiti na wadau wa afya kutoka nchi zaidi ya 60 barani Amerika na Asia wanatarajiwa kukutana jijini Dar es Salaam katika Mkutano wa Kimataifa wa Heart Team Africa Cardio Imaging 2026, utakaofanyika kuanzia Juni 4 hadi 6, 2026. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dk. Peter Kisenge, amesema mkutano huo wa nne utafanyika katika Hoteli ya New Sapphire, Mbezi Beach, na unalenga kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya afya, hususan magonjwa ya moyo. Dk. Kisenge amesema mkutano huo utatumia mbinu za kisasa za uchunguzi na vipimo vya afya ya moyo, huku ukiwa pia fursa ya kuonesha maandalizi ya Tanzania katika kupokea wageni wa kimataifa, ikiwemo kuelekea mashindano ya AFCON. “Kupitia mkutano huu tutashirikiana na taasisi mbalimbali za kimataifa ikiwemo za Andalusia, na k...

TNCC YAZINDUA SERA YA MAZINGIRA, KUCHOCHEA BIASHARA YA UCHUMI WA KIJANI

Image
TNCC Yazindua sera ya mazingira, yachochea biashara endelevu na uchumi wa kijani Dar es Salaam KATIKA kuimarisha ulinzi wa mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi katika sekta ya biashara, Chemba ya Taifa ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TNCC) imezindua Sera ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi ya mwaka 2026, inayolenga kuhimiza ufanyaji wa biashara endelevu na chanya nchini. Akizungumza na Habari leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi huo, Rais wa TNCC, Vicent Minja, amesema sera hiyo ni nyenzo muhimu itakayozisaidia biashara kuwa sehemu ya suluhisho la changamoto za mazingira, huku zikiendelea kuchangia kukuza uchumi wa taifa. Amesema kupitia sera hiyo, TNCC inalenga kuweka misingi ya Sustainable Business Practices zitakazohakikisha ukuaji wa uchumi unakwenda sambamba na uhifadhi wa mazingira na matumizi bora ya rasilimali. “Sera hii inalenga kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika biashara rafiki kwa mazingira, kupunguza taka na kuch...

TAMASHA LA PASAKA KUFANYIKA APRILI 5, 2025 MIKOA 20

Image
Wasanii nguli wa nyimbo za Injili kutoka mataifa mbalimbali wanatarajiwa kuungana na waimbaji wa Nyimbo za Injili hapa nchini kutumbuiza katika Tamasha la Pasaka ambalo huandaliwa na kuratibiwa na Kampuni ya Msama Promotions ambapo kwa msimu huu linatarajiwa kufanyika kwa mikoa 20 likianzia na Mkoa wa Dar es Salaam. Mapema akizungumza na waandishi wa Habari Mkurugenzi wa Msama Promotions Alex Msama amesema msimu huu wa pasaka Tamasha hilo litaanza tarehe 5 ya mwezi wa nne,likizunguka katika mikoa 20,kutoa burudani likiwa limesheheni wasanii mbalimbali wakubwa kutoka Tanzania na nje ya Tanzania lengo ikiwa ni kuwapa burudani waumini wa dini ya kikristo na wasio wa kristo sambamba na kutoa ujumbe wa kiroho. Kadhalika Msama amesema wasanii wakubwa wanatarajiwa kupanda katika majukwaa hayo kutoa burudani kabambe kwa mikoa 20 kwani hiyo ni dhamira ya wao kama waandaji kuwapa burudani waumini wa Injili. Ikumbukwe Tamasha hilo ambalo huandaliwa na Msama Promotions limekuwa maarufu k...