Posts

Showing posts from June, 2024

SERIKALI KULETA MAPINDUZI KATIKA TASNIA YA HABARI

Image
SERIKALI inakusudia kushirikiana na sekta binafsi kufanya mabadiliko na maboresho makubwa kwenye sekta ya habari kwa kutunga na kuhuisha sera, sheria, miongozo inayosimamia sekta za habari, mawasiliano na teknolojia ya habari. Serikali pia inakusudia kuimarisha huduma za mawasiliano ya simu na posta kote nchini kwa kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kukuza na kuimarisha biashara mtandao nchini, kuimarisha miundombinu itakayowezesha utekelezwaji wa uchumi wa kidigitali, kuimarisha ulinzi na usalama wa anga. Hayo yamesemwa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Thobias Makoba ambaye alimwakilisha Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye leo Juni 27,2024 kwenye kongamano la uhuru wa kujieleza na sheria za vyombo vya habari lililoandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC). Msemaji huyo wa Serikali amesema mwaka 2024/2025 Wizara imepanga kukamilisha uhuishwaji wa sera mbalimbali ikiwamo sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003 na kutunga Sera mpya ya Taifa ya...

COSOTA YASISITIZA KAMPUNI YA WASANII WA FI LAMU

Image
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (Cosota) Doreen Sinare  amewasihi wadau wa filamu kuhakikisha wanaanzisha Kampuni za Kukusanya Mirabaha(CMOs) ili waweze kunufaika zaidi. Tayari wasanii wa muziki wana kampuni yao ya kukusanya mirabaha iliyozinduliwa tangu mwaka jana na imeanza mchakato wa ukusanyaji ya mapato ya wasanii kwenye mitandao na vyombo vyote vinavyotumia kazi za sanaa. Akizungumza Dar es Salaam kwenye mkutano wa wadau kukusanya maoni ya itifaki ya Beijing Sinare amesema wanategemea wasanii hao wa filamu wataanzisha kampuni yao itakayofanya kazi  kwa uchungu. "Nawadai Kampuni inayosimamia masuala ya filamu na tumebadilisha Sheria ya mwaka 2022 kuruhusu wadau wa makundi yale yanayoendana  yaweze kufanya kazi zake, sisi tutakimbizana upande wa sera, kutoa elimu, kuwawekea mazingira mazuri ya sheria, kanuni na taratibu,"amesema. Amesema:"Haya masuala ya kukusanya mirabaha inabidi myafanye nyie mtakuwa na uchungu zaidi ya sisi tunavyofanya" A...

WASANII WATAKIWA MAONI

Image
Serikali kupitia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imewataka wasanii kushiriki kikamilifu katika utoaji wa maoni ya maboresho ya itifaki ya Beijing ya 2012  kwa kuwa ni mpango uliolenga kuwanufaisha. Hayo yamesemwa Dar es Salaam na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Sanaa wa Wizara hiyo Venance Mwamengo wakati akifungua mkutano wa wadau wa ubunifu kujadili itifaki hiyo, ulioandaliwa na Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (Cosota) kwa kushirikiana na Shirika la Miliki Bunifu la kikanda la Afrika (ARIPO). Amesema  ushiriki wao kwa pamoja ni kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan ambaye anataaka kuona maamuzi shirikishi. "Serikali ina wajibu wa kuhakikisha kuwa wasanii na wabunifu wanalindwa na sheria na wananufaika ndio maana imeweka mazingira rafiki ili kuhakikisha wasanii, waandishi na wabunifu wananufaika na Sheria ya Hakimiliki na haki bunifu kwa hivyo ni muhimu washiriki kutoa maoni,"amesema. Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Cosota Doreen Sinare amesema w...

FAINI NI MUHIMU ZINAPASWA KUHESHIMIWA

Image
  RAIS wa Chama cha Wanasheria Afrika Mashariki, Fauz Twaib amesema fani ya sheria ni muhimu katika taifa lolote hivyo inapaswa kuheshimiwa. Twaib amesema hayo alipokuwa mgeni rasmi katika Siku ya Taaluma ya Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ( UDSM). "Umuhimu wa uanasheria na kuwepo kwa wanasheria ndiyo inayofanya fani hii kuwa muhimu. "Wanasheria tuna nafasi muhimu katika maisha ya binadam hivyo tutumie vizuri nafasi hiyo kwa kufanya yale ambayo jamii inahitaji tufanye. Tuna wajibu wa kijamii wa kuwekeza kutumia kile tulichonayo," amesema. Pia Twaib alielezea uzoefu wake katika fani hiyo, ambapo alisema alianzia kazi ya ualimu katika shule ya msingi, akajiendeleza na kuwa mhadhiri wa sheria UDSM. baadaye alikuwa wakili kisha akateuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na sasa ni Rais wa Chama cha Wanasheria Afrika Mashariki. Naye Mratibu wa Masomo ya Degree ya Awali kutoka Shule Kuu ya Sheria UDSM,  Dk Florencia Kimario alisema katika siku hiyo wanafunzi wanakutana na watu m...

MADADA POA WAFIKISHWA MAHAKAMANI

Image
WATUHUMIWA 24 kati ya 36 waliokamatwa Kwa kosa la kuuza miili yao maarufu kamà "dada poa" wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Sokoine Drive wakikabiliwa na tuhuma za kufanya vitendo venye mazingira ya umalaya. Akizungumzia mazingira ya shauri hilo  baada ya  kutajwa, Wakili anayetetea kundi Hilo ,Peter Madeleka amesema  Kwa sababu ambazo hazijafahamika watuhumiwa hao pekee ndio walifikishwa Mahakamani hapo. Amesema watuhumiwa 18 wamefikishwa mbele ya Hakimu Janeth Mgaya na baada ya kusikiliza maelezo upande wa serikali,Hakimu alisema shauri liko wazi Kwa dhamana Kwa ajili ya washtakiwa wote 18 kwa dhamana ya Kila Mmoja kutoa fedha taslimu sh 300,000. Madeleka amesema  pamoja na dhamana hiyo lakini inadaiwa kuwa Hakimu alikuwa na dhamira ya kuona Haki inakwama na kwa mujibu wa Ibara ya 13(c) na (b) ya Katiba  yeye mwenyewe ameamua kuwalipia dhamana watuhumiwa 18 kwa  kiwango Cha sh milioni 5.4. Aidha amesema  watuhumiwa wengine watano,wamepe...

WAZIRI MKUU AZINDUA VITABU VYA HISTORIA YA BUNGE

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua vitabu vya historia ya Bunge ambavyo vitasaidia kuhamasisha tafiti na kujua zaidi kuhusu mchango wa Bunge katika maendeleo ya jamii nchini. Amesema kuwa vitabu hivyo pia vitakuwa kielelezo cha mafanikio na changamoto ilizopitia Bunge la Tanzania katika kudumisha demokrasia na utawala wa sheria. “Historia yetu ni sehemu ya mchango wetu kwa jumuiya ya kimataifa katika kukuza amani, utulivu na maendeleo.” Amesema hayo leo (Jumatano, Juni 26, 2024) wakati wa uzinduzi wa vitabu viwili vya historia ya bunge katika ukumbi wa Pius Msekwa, Jijini Dodoma.Vitabu vilivyozinduliwa ni Kitabu cha Historia ya Bunge kutoka 1926-2024 na Wabunge wa Tanzania na nafasi zao kuanzia mwaka 1965-2023 “Kumbukumbu za historia ya Bunge zinaweza kuchochea utafiti wa kitaaluma na maendeleo ya nadharia za kisiasa na utawala. Watafiti wanaweza kutumia taarifa hizi kujenga ufahamu mpya na kupendekeza mifumo bora ya kisiasa.” Kwa upande wake Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amepong...

TAMASHA LA HIP HOP ASILI KUFANYIKA PWANI

Image
Msanii wa muziki wa HipHop Asili Festival kwa kushirikiana na ubalozi wa Ufaransa umeaanda tamasha la kimataifa la  Hip Hop asili lenye lengo la  kukuza utamaduni na ushirikiano likionyesha uridhi wa kipekee wa sanaa  Tamasha hilo litafanyika Mkoani Pwani Bagamoyo katika Chuo cha sanaa cha TASUBA ambapo kutakuwa na muunganiko wa talanta za kitaifa na kimataifa katika utamaduni wa HiP HoP Hayo ameyasema Ofisa Matei Babis Mkurugenzi wa Hip Hop Asili jana usiku kwenye Mkutano na waandishi wa habari ulifanyika Jijini Dar es salaam Matei Amebainisha kwa kusema kutakuwa na asili band ambapo wanamuziki na wasanii wa kughani mashairi wameshirikiana kuunda mchanganyiko wa pekee wa hiphop lakini pia kutakuwa na upigaji midundo  kwa mdomo yaani ( Beatbox) Ameongezea kuwa mbali na hayo kutakuwa na kutambulishwa kwa  (Breaking )kama mchezo wa Olimpiki pamoja na maonyesho ya sanaa ya machata (Graffiti) ambapk kuta za TASUBA zitapendezeshwa kwa usanifu wa graffiti kutoka kwa W...

MAMIA WAJITOKEZA KUPATA HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA

Image
Mamia ya Wananchi wa Wilaya ya Kinondoni na maeneo ya Jirani wamejitokeza kwa wingi kupata huduma ya msaada wa kisheria bure iliyotolewa na Shirika la Citizen Foundation kwa kushirikiana na Mama Samia legal Aid Campaign katika viwanja vya Tanganyika Packers - Kawe Jijini Dar-es-Salaam. Akizungumza wakati wa utoaji wa huduma hiyo leo tarehe 22 - Juni 2024;  Mkurugenzi wa Mama Samia legal Aid Campaign Bi. Ester Msambazi amesema Wananchi wamejitokeza kwa wingi hali inayoonesha kuwa ipo haja kwa watoa huduma za msaada wa kisheria kuwafuata Wananchi badala ya kuwasubiria maofisini. Amesema “Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni namba moja katika utoaji wa huduma za msaada wa kisheria kwani yeye ndiye kiongozi wetu pale juu kwenye huduma hizo lakini Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pindi Chana, katibu Mkuu Bi. Mary Makondo lakini na wadau wengine ambao ni Wanawake wanaonesha juhudi za pamoja kama Wanawake katika kuunga mkono  juhudi za Mhe Rais  Dkt. Samia kuhakikish...

RAIS SAMIA MGENI RASMI TWENZETU SONGWE

Image
  Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatajarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye tamasha la kimataifa la utamaduni litakalofanyika Mkoani Ruvuma . Tamasha hilo ambalo litafanyika kuanzia tarehe 20 mpaka 27 Mkoani humo linatarajia  kufungua fursa mbalimbali, katika nyanja ya  kiutamaduni, kiutalii, pamoja na upatikanaji wa mapato. Hayo ameyasema Naibu wa waziri wa utamaduni sanaa na michezo Hamis Mwinjuma leo Juni 20,2024  Katika ufunguzi wa tamasha hilo Jijini Dar es salaam  Mwinjuma amesema tamasha hilo litakuwa la kihistoria kwani wageni wengi wanatarajiwa kutoka nje na ndani ya nchi na itawakutanisha makabila zaidi ya 120 nchi nzima . Awali akiongea muandaaji wa Tamasha hilo Mwesigwa Selestine kutoka Drum- Beats amesema tamasha hilo limekuwepo kwa takribani mwaka wa tatu na lina lengo la kutunza pamoja na kuhifadhi utamaduni pamoja na asili ya mtanzania . Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya twenzetu Ruvuma twenzetu Songwe.

VIONGOZI WA DINI WAOMBA TWITTER KUFUNGIWA

Image
  Viongozi wa Dini nchini wamezitaka Mamlaka za serikali kuufungia mtandao wa Kijamii wa X ambao zamani ulijulikana kama Twitter Kwa kuhamasisha vitendo vya mapenzi ya jinsia moja (ushoga) Akizungumza na waandishi wa Habari leo juni 11, 2024 Jijini Dar Es Salaam Alhaj Dkt Abdul Suleiman amesema kwamba vitendo vya ushoga vimepigwa vita hata katika maandiko ya dini,hivyo vitendo hivyo havikubaliki na vinapaswa kulaaniwa. Dkt Sule amesema kwamba kufuatia mtandao wa X (Twitter)kuruhusu kuchapisha maudhui yanayohamasisha vitendo vya mapenzi ya jinsia moja ikiwemo ushoga na usagaji Mamlaka zinazohusiana na mawasiliano zinatakiwa kuchukua hatua haraka iwezekanavyo ikiwemo kuufungia kabisa mtandao huo. Kwa upande wake Askofu na Katibu mkuu wa Kanisa la Methodox Tanzania Allen Siso amesema katika vitabu vya dini vyote havikubaliani na ndoa za jinsia moja akitolea mfano kitabu cha Warumi 1:26 kinachosema 'hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu,hata wanawake wakabadili matumizi ya as...

BENKI YA TCB YATANGAZA MAFANIKIO

Image
MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya Biashara Tanzania (TCB), Adam Mihayo, amesema benki hiyo imeshuhudia ongezeko kubwa la mapato ya jumla kwa Sh. Bil. 19.27 sawa na asilimia 11.19 hadi kufikia Sh. Bil. 192.1 ikilinganishwa na mwaka 2022 mapato yalikuwa Sh. Bil. 172.83 sawa na asilimia 1.72. Aliyasema hayo wakati alipozungunza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu Mkutano Mkuu ambapo katika mkutano huo aliwasilisha taarifa ya fedha ya mwaka 2023. Mihayo, alisema kupitia mipango yake ya kimkakati na ubunifu, benki imedhihirisha mafanikio makubwa ya kifedha na ya kiutendaji. “Ndani ya mwaka 2023, mali za TCB Benki ziliongezeka kutoka Sh. Trilioni 1.285 mwishoni mwa mwaka 2022 hadi Sh. Trilioni 1.389 mwishoni mwa mwaka 2023 sawa na ongezeko la asilimia 8.1 sawa na Sh. Bil. 103.9. “Jumla ya mikopo yote iliongezeka kwa Sh. Bil. 73.1 kutoka Sh. Bil.839 mwishoni mwa mwaka 2022 kufika Sh. Bil. 911.2 mnamo Desemba 31, 2023 ikionesha ongezeko la asilimia 8.72,”alisema Mihayo. Mihayo, al...

SILENT OCEAN CONSUMER CHOICE AWARD AFRICAIMEZINDULIWA RASMI

Image
Tuzo za Chaguo la Wateja Afrika (CCAA) litashirikisha biashara na chapa kutoka nje ya nchi, linatarajiwa kufanyika mwaka huu Novemba katika ukumbi wa The Super Dome. CCAA pia inajulikana kama Silent Ocean Consumer Choice Award Africa ni chachu ya kupaza sauti za watumiaji na kuridhika na huduma na bidhaa mbalimbali sokoni. Ni jukwaa la Afrika la utambuzi wa biashara na ushirika kwa watoa huduma wa bidhaa na huduma kupitia kura za watumiaji. Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua msimu mpya Mwanzilishi na Mkurugenzi wa CCAA, Diana Laizer, alisema kuwa wafanyabiashara kutoka Afrika Kusini, Kenya, Malawi, Nigeria, na nchi nyingine wanatarajiwa kuteua chapa zao katika hafla ya inayotarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu. "Tukio la mwaka jana lilikuwa na vipengele vikuu 22 na vijamii 70 katika mkutano huo. Vipengele hivyo vinajumuisha vifaa, mawasiliano ya simu, usafiri wa anga, huduma za kifedha, mali isiyohamishika, bima, mafuta na gesi, hoteli na ukarimu, usalama, bidha...

VEE KASHERA HAKUNA WA KUNITENGANISHA NA AZIZI KI

Image
MSANII wa Filamu za kibongo, Vanessa Kashera maarufu 'Vee Kashera' ameibuka na kudai kwamba mwanamitindo Hamisa Mobetto hawezi kuvunja mahusiano yake na kiungo mshambuliaji wa Yanga, Stephane Aziz Ki sababu kila mtu ana nafasi yake kwa mchezaji huyo. Vee Kashera amesema Aziz Ki, mtu wake wa karibu na mahusiano yao ni urafiki sio kama watu wanavyosema juu ua kiungo huyo kwa wako kwenye mapenzi. "Mashabiki ndio wanaozusha kuwa  ni wapenzi hakuna sehemu tuliyoweka wazi jambo hilo kokote, hakuna mtu anaweza kuchukua nafasi yangu kwa Aziz Ki kila mtu ana urafiki wake kwa nafasi yake, nina muda wangu kwa Aziz K na Hamisa atakuwa na muda wake." Amesema mrembo huyo Kuhusu kwenda uwanja wa Benjamini Mkapa siku Yanga wakikabidhiwa kombe, amesema hakujisikia kwenda kwenye sherehe za kukabidhiwa za ubingwa  sababu alikuwa na mambo yake mengine. "Nilikuwepo kwenye siku ya kuzaliwa kwa Hamisa alikuwepo kwenye sherehe za Yanga, sikutaka kwenda yule dada alienda Azizi KI ana mar...

CAREEN SIMBA PACOME NI MSHKAJI TU

Image
MREMBO Careen Simba amekana kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mchezaji Pacome  Zouzoua kama tetesi zilivyosambaa. Careen amesema  ashangazwi na maneno ya mashabiki wala hayamuumizi kwa kuwa hata Pacome anafahamu kuwa wao ni marafiki na ni shabiki yake mkubwa. "Pakome sio mpenzi wangu ni mchezaji wa kigeni na ni rafiki yangu mkubwa lakini pia mimi ni shabiki yake mkubwa mambo ya mapenzi ni uzushi wa mitaani" alifafanua Caren "Maneno yanayoongelewa mitandaoni kuwa Pacome ni mpenzi wangu hayo ni maneno yao na wala hayaniumizi kichwa." Aidha ameongeza kuwa "Bongo ukishakuwa maarufu ukaonekana na mtu fulani basi umeyaruhusu maneno kwangu ni kawaida sisi ni washikaji tu."amesema Careen Simba

MOSE IYOBO HAKUNA WA KUNITENGA NA COOKIE

Image
Dansa kwenye video za wasanii wa Bongo fleva Moses Iyogo 'MoseIyobo' amesema kuwa hakuna mtu anaweza kuchukua nafasi yake kwa mwanae  Cookie hapa duniani. Akijibu swali kuhusiana na mwanae kupewa zawadi ya gari huku yeye akitumia muda nae mwingi kufundisha kucheza nyimbo za wasanii, amesema kuwa atabaki kuwa baba Cookie tu. "Baba ni baba hakuna anayeweza kumbadili mtu kuwa mzazi wa Fulani na kuhusu gari aliyozawadiwa na mama yake Cookie sidhani kama anapanda hiyo gari chunguzeni vizuri mtapata majibu." "Hakuna zawadi nzuri duniani kwa mzazi kumpa mwanae kama Upendo ni kitu kikubwa sana kwa kumpa mtoto wako, Kuna watoto  wamekosa upendo wa wazazi ndio sababu nampatia mwanangu."amesema Mose Aidha ameongeza kuwa "hakuna kitu kinachoweza kutenganisha mtoto na mzazi wake kwa namba yoyote Cookie niwanangu nampenda na ananipenda." "Ninachojua natimiza majukumu yangu kama mzazi kuhusu huo zawadi gani nimpatie mwanangu sipangiwi na mtu nimpe nini mwana...

RAY GABO NA DUMA SIO LEVEL ZANGU

Image
Msanii wa Filamu nchini Vincent Kigosi 'Ray' anashangazwa na watu kulinganishwa na Gabo na Duma ameomba kutoshindanishwa na msanii yoyote nchini. Amesema kuwa ameshafanya makubwa katika Tasnia hii na sasa yeye yupo kimataifa. Ray amesema hayo Jijini Dar es Salaam na kudai kuwa wasanii wanaofanya vizuri asilimia 90 amewatoa yeye hivyo Mwalimu hawezi kulinganishwa na mwanafunzi wake. "Watu wanashindwa kutofautisha kwa sasa si shabiki sio nani naomba sitaki kushindanishwa na msanii yoyote yule nafasi yangu kwa sasa ni wasanii wa Kimataifa. "Nishachukua tuzo nchini Kenya, Uganda hadi Nigeria halafu Bado unataka kunilinganisha na wasanii wa juzi niliowaleta mwenyewe kwenye tasnia hapana kwa kweli." "Asilimia 90 ya wasanii unaowajua wewe hapa nchini Tanzania nimewatambulisha na kuwaleta kwenye tasnia ya filamu sasa unawezaje kumfananisha Mwalimu na mwanafunzi hao kina Gabo washindanisheni na kina Duma ila sio Ray sio level zangu kabisa."amesema Ray

HAMISA NIPO SINGO AZIZI KI SIO MPENZI WANGU

Image
MREMBO na mwanamitindo, Hamisa Mobetto amesema kwa sasa hana uhusiano wa kimapenzi na mwanaume yoyote. Hamisa amesema kuwa ameamua kujipa muda na kufanya kazi zake hadi hapo atakapoamua tena kuingia kwenye mapenzi. Pia amekanusha madai ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mcheza soka wa timu ya Yanga Aziz Ki. “Sidhani kama kuna mishikano kama baadhi ya watu mnavyosema tulivyoonekana, chochote kilichokuwa kinaendelea pale ni cha kawaida, kama ungeniona na mtu mwingine mimi nipo singo nimeamua kujiba muda“ Ikumbukwe kuwa taarifa za Mobetto na Aziz KI kuhusishwa kimapenzi yalianza baada ya Hamisa kujumuika na wachezaji wa Yanga walipokabidhiwa Kombe la Ligi Kuu ya NBC uwanja wa Mkapa.

MTANDAO WA X KUFUNGIWA TZ

Image
Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umeiomba Serikali kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kuufungia mtandao wa Twitter (X) kutokana na maudhui yake kutokuendana na mila na desturi za kitanzania . Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa UVCCM, Mohamed Kawaida wakati akizungumza na waandishi wa habari. Amesema dhamira ya maudhui ya mtandao wa Twitter maarufu X kwa sasa ni mbaya kutokana na kutokwendana na tamaduni za kitanzania. “UVCCM imekuwa na utamaduni na kazi ya kuendelea kufatilia malezi ya vijana wa kitanzania wote ambapo hivi karibuni imepokea taarifa kuwepo Kwa mtandao wa X wenye maudhui ya kingono,” amesema. Kawaida amesema kupitia Serikali Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikifungia mitandao yote yenye maudhui ya namna hiyo hivyo anaimani pia itaufungia mtandao huo. “Sasa wakati umefika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuufungia mtandao huo kutokana na maudhui yake kutokwendana na mila na destu...

MISS TANZANIA HALIMA BADO YUPO YUPO

Image
Mwana FA unaoa lini? (Bado nipo nipo kwanza) Unasema? (Bado nipo nipo sana)Mwana FA unaoa lini? (Bado nipo nipo mwana) Eeh? (Wa kuoa ntakuwa mimi mwana!?) “Mwana FA unaoa lini? (Bado nipo nipo mama) Unasema? (Bado nipo nipo sana) Mwana FA unaoa lini? (Bado nipo nipo kwanza) Eeh! (Wa kuoa ntakuwa mimi mama!?),” huo ni wimbo Bado Nipo Nipo Kwanza wa msani Hamis Mwinjuma a.k.a Mwana FA, ambaye sasa ni Mbunge wa Muheza na Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mwana FA alikuwa akizungumzia kuhusu ndoa, kwamba bado hajafikiria, sasa achana na Mwana FA, hebu mgeukie Miss Tanzania mwaka 2023, Halima Kopwe naye amekuja na staili kama ya Mwana FA, akidai kutokana na wingi wa kazi anazofanya muda wake ni mchache, hivyo hawezi kujihusisha na masuala ya mapenzi kwa sasa. Halima amesema kwa sasa bado anaendelea na kazi zake, hivyo hatoweza kuingia katika mahusiano na yeyote hadi atakapomaliza kazi zake mwaka wowote. “Muda mwingi nimekuwa katika project zangu na muda wa kuingia katika mahusian...

AGAPE BENDI KUNOGESHA TWENZETU KWA YESU.

Image
BENDI ya Agape Gospel inatarajiwa kunogesha Tamasha Twenzetu kwa yesu Katika Viwanja vya Tanganyika  Peackers Juni 15 Mwaka huu jijini Dar es Salam . Akizingumza na Waandishi wa Habari jijini Naibu KatibuMkuu Dayosisi Mashariki na Pwani (KKKT) Willbroad Mastai amesema Bendi hiyo inayo sifika na Wimbo wa Hallo mbiguni, inatarajia kunogesha tamasha twenzetu kwa yesu ikiwa na lengo la kuwa kutanisha Vijana waweze kumtumikia Mungu na kuepukana na Uovu. "Neno la Mungu linasema Hutuponya nakutoa katika Maangamizo yote,Twenzetu kwa yesu tuna kuja na ujumbe Uwe nuru katika Maisha yako"Alisema Naibu Katibu Mkuu DMP Willbrod Mastai. Willbrod Mastai aliongeza kuwa sambamba na Bendi hiyo Waimbaji wengine nipamoja Nakibonge wa yesu. Alisisitiza kuwa katika Tamasha hilo vijana wanaotarajiwa kuhudhuria tamasha hilo 30,000 ambapo Dhumuni la tamasha hilo nikuwabadilisha Vijana kitabia kupitia Neno la Mungu. "Kupitia Utumishi wa Neno la Mungu tunategemea Kumpata kijana anayejiepusha na uo...

Sahara Consult and the Mastercard Foundation EdTech Fellowship

Image
Sahara Consult and the Mastercard Foundation EdTech Fellowship  reveal thefirst cohort of10Start-ups setto transform Tanzania’s education sector  Dar es Salaam, Tanzania –June 7, 2024Sahara Consulthas named the10homegrown Tanzanian  EdTech companiesthat will be acceleratedas part ofits inaugural partnership with the Mastercard  Foundation EdTech Felowship. The Fellowship is an acceleration program designed to support promising African EdTech ventures in  partnership with innovation hubs and accelerators across the continent.In 2023, solutionsbyFellowship  cohorts in South Africa, Nigeria, and Kenya reached 2.6 million learners. Over the next eight months, Tanzania’s inaugural cohort of growth-stage EdTech companies willbenefit  from Sahara Consultmentorship through business and financial support and insight into the science of  learningto preparethem for scale, sustainability, and impact.  “Congratulations tothe tenEdTech companies. This mark...

TGNP WAICHAMBUA BAJETI

Image
Mwenyeki wa Bodi ya Mtandao wa jinsia  nchini(TGNP),Gemma Akilimali,amesema ili bajeti ya mwaka  2024/2025 ikizi matakwa ya watanzania inatakiwa ishirikishe makundi yote. Akilimali amesema hayo leo mapema jijini Dar es salaam wakati akitoa maoni juu ya Bajeti ya mwaka 2024/2025 inayowasilishwa na Waziri wa Fedha,Dkt Mwigulu Nchemba Bungeni Dodoma. Amesema kumekuwa na changamoto kuhusu  Bajeti zinazowasilishwa zimekuwa haziki matakwa ya makundi yote. "Upungufu ambao tunaona ni ushikirishwaji toka chini na jinsi gani wananchi wanapewa kipaumbele"Amesema Akilimali. Akilimali ambaye ni mwanaharakati wa siku nyingi wa kutetea haki za Wanawake nchini,ameomba Bajeti hii iende kutatuj changamoto zinazomkabili Mtanzania na isiwe ya kisiasa. Amesema bado Mtanzania anakumbana na Changamoto zinazomkabili na kutaka bajeti ikaenda kutatua matatizo. Kwa Upande wake Mkurugenzi wa TGNP Mtandao,Lilian Liundi,ametaka Bajeti iliyowasilishwa ijikite katika kutatua changamoto vifo vya Mama na ...