HEINEKEN YATANUA WIGO ZAIDI
Heineken yapanua wigo zaidi, Yatangaza uzinduzi wa bidhaa zake mpya mbalimbali kwenye orodha ya jadala lake nchini Tanzania. Kampuni inayoongoza duniani ya vinywaji, Heineken imesherehekea upanuzi wake zaidi wa vinywaji na kutangaza bidhaa mpya ikionyesha orodha za aina mbalimbali za chapa zilizoanzishwa nchini Tanzania katika hafla ya kipekee iliyofanyika jijini Dar es salaam siku ya Jumamosi, Mei 25, 2024. Hii inafuatia kukamilika kwa ununuzi wa kampuni ya Distell Group Holdings Limited (‘Distell’) na Namibia Breweries Limited (‘NBL’). Waliohudhuria kwenye hafla hiyo ni wageni waalikwa, viongozi wa tasnia na wawakilishi wa vyombo vya habari, pamoja na Mgeni Rasmi, Mhe. Prof. Kitila A.K Mkumbo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji. Wageni wengine mashuhuri waliuhudhuria katika kuadhimisha hatua hiyo muhimu kwa Kampuni ya Heineken Beverages Tanzania ilipozindua bidhaa zake za kusisimua katika soko la Tanzania. Meneja Mkazi wa Kampuni ya HEINEKEN nchini, Obabi...