FLAVIANA MATATA FOUNDATION WAJENGA NA KUKABIDHI MATUNDU 12 YA VYOO SHULE YA MANYUNYU
WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imezindua na kukabidhi mradi wa matundu 12 ya vyoo, sehemu ya kunawia mikono, chumba maalumu kwa wanafunzi wenye mahitaji, chumba maalum kwaajili ya wasichana kujisitiri, pamoja na sehemu ya kuchomea taka hususani taulo za kike zilizokwisha kutumika uliotekelezwa na Taasisi ya Flaviana Matata kwa ufadhili wa SEGAL FAMILY FOUNDATION na MFADHILI MWINGINE, katika shule ya sekondari Manyunyu iliyopo mkoani Njombe. Mradi huo utanufaisha jumla ya wanafunzi takribani 910 kila mwaka katika shule ya sekondari Manyunyu na sambamba na hilo miundombinu hiyo itatatua changamoto ya muda mrefu ya uhaba wa vyoo,kichomea taka na upatikanaji wa maji shuleni hapo. Hafla ya Uzinduzi huu imehudhuriwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Flaviana Matata, Bi. Flaviana Matata akiambatana na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Njombe akiwemo Mkuu wa Mkoa, DAS , Mkurugenzi wa halmashauri , pamoja na mashirika na wadau mbalimbali ambao wanatekeleza miradi ya maji na usimamizi wa usafi ya...