MAVUNDE AONGOZA MKUTANO CHAMA CHA MIGODI
WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde ameongoza mkutano maalum baina ya Serikali na Chama cha Migodi Tanzania, ambapo wadau wote wa sekta ya madini wamekutana kujiandaa kwa maonesho yatakayofanyika mjini Cape Town, Afrika Kusini.
Madhumuni ya mkutano huo ni kuiwakilisha Tanzania kwenye jukwaa la kimataifa na kuvuta uwekezaji, hususan katika maeneo ya utafiti, na kuongeza ushiriki wa Watanzania katika huduma na usambazaji wa bidhaa mbalimbali.
Waziri Mavunde amesisitiza umuhimu wa sauti moja kati ya Serikali na sekta binafsi katika kuitangaza nchi nakuonyesha matumaini kuwa fursa hii italeta uwekezaji mkubwa, kuongeza ajira kwa Watanzania, na kuchangia katika kuongeza mapato ya taifa.
Hii ni mara ya kwanza kwa Serikali na sekta binafsi kukaa chini pamoja kwenye mkutano wa namna hii, na inaashiria hatua muhimu kuelekea ushirikiano wenye tija.
Madhumuni ya mkutano huo ni kuiwakilisha Tanzania kwenye jukwaa la kimataifa na kuvuta uwekezaji, hususan katika maeneo ya utafiti, na kuongeza ushiriki wa Watanzania katika huduma na usambazaji wa bidhaa mbalimbali.
Waziri Mavunde amesisitiza umuhimu wa sauti moja kati ya Serikali na sekta binafsi katika kuitangaza nchi nakuonyesha matumaini kuwa fursa hii italeta uwekezaji mkubwa, kuongeza ajira kwa Watanzania, na kuchangia katika kuongeza mapato ya taifa.
Hii ni mara ya kwanza kwa Serikali na sekta binafsi kukaa chini pamoja kwenye mkutano wa namna hii, na inaashiria hatua muhimu kuelekea ushirikiano wenye tija.

Comments
Post a Comment