FAMILIA KUMKUMBUKA KOMBA KIVINGINE
Katika kumuenzi aliyekuwa muimbaji na mtunzi mahiri wa nyimbo za kijamii na kisiasa Captain John Damiano Komba familia imeandaa mkakati maalum kumuenzi Captain Komba
Wakizungumza na waandishi wa habari wawakilishi wa familia ya Captain Komba wamesema mara nyingi hufanya kumbukizi ya kumuenzi Captain kila mwaka lakini kwa mwaka 2024 wangependa kuwa tofauti ambapo mwaka huu wamedhamiria kuungana na Rais Samia pamoja na Serikali kusapoti matibabu ya watoto wanaosumbuliwa na ugonjwa wa moyo na kujenga Makumbusho ya Captain Komba (Museum)

Comments
Post a Comment