Posts

Showing posts from September, 2025

PIMEA USIKU WA WANA NDOA ULIVYOFANA MSIFICHANE NA KUWEKEANA VITU

Image
‎Wanandoa watashauriwa kuwa na mitoko ya pamoja kujua mwenzio anapenda kula nini kuvaa na kunywa ili kuendelea kudumisha ndoa yao, Ndoa bora ni ushirikiano, siyo mashindano. ‎Akizungumza mwaandaaji wa Usiku huo wa wanandoa The Pinnacle of Mentorship & Excellence Award (PIMEA) Dkt Christine Mbelwa amesema Lengo la Usiku wa Wanandoa nikuwakutanisha na kubadilishana mawazo kuhusiana na kukumbusha baadhi ya mambo ya ndoa. ‎"Moja ya majukumu ambayo Mungu amenikabidhi mimi pamoja na mume wangu ni kujenga ndoa na mahusiano imara kupitia uandishi wa vitabu, semina, makongamano na mafundisho mbalimbali. ‎"Usiku wa Wanandoa ni moja ya jukwaa kuu tunalotumia kwa lengo la kuboresha, kuponya na kuokoa ndoa. Tunawakusanya wanandoa pamoja, kuwapa mafundisho ya vitendo ana kwa ana, kuruhusu maswali na kutoa majibu ya moja kwa moja. ‎ ‎Amesema Zaidi ya mafundisho, wanandoa hupata nafasi ya kufurahi pamoja kwa kushiriki vinywaji, michezo na burudani mbalimbali. Shughuli hi...

REPORI YA HABARI ZA MATUMIZI YA NISHATI YA SOLA KATIKA KILIMO YAZINDUA RASMI

Image
Habari za Matumizi ya Nishati ya Jua Katika Kilimo Zaongezeka kwa 79% Afrika Mashariki Brighitter Dar es Salaam. Ripoti mpya imebainisha ongezeko la asilimia 79 ya habari zinazohusu matumizi ya nishati ya jua katika kilimo Afrika Mashariki, kutoka habari 63 mwaka 2023 hadi 113 mwaka 2024. Ripoti hiyo imeonesha magazeti kuongoza kwa utoaji wa habari hizo kwa asilimia 65.1, huku Tanzania ikishika nafasi ya tatu nyuma ya Kenya na Uganda kwa uzalishaji wa maudhui. Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, alisema ongezeko hilo linatokana na mafunzo ya waandishi kuhusu nishati safi katika kilimo, yaliyofanyika mwaka 2023. Balile alisisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kusukuma ajenda ya nishati safi kwa ajili ya kusaidia kilimo endelevu, hasa katika maeneo ya umwagiliaji na uhifadhi wa mazao. Ripoti hiyo iliwasilishwa na Dk. Darius Mukiza wa ACME, akieleza kuwa waandishi 47 walipatiwa mafunzo kupitia vyombo sita kutoka Tanzania, Kenya na Uganda. Kenya i...

MSAMA AWAJIA JUU WANAOTAKA KUVUNJIKA KWA AMANI

Image
Mkurugenzi wa Msama Promotions Alex Msama ametoa wito kwa wale wanaokuwa mstari wa mbele kuhamasisha uvunjifu wa amani kwa nchi kupitia majukwaa ya mitandao ya kijamii, kuelewa kwamba Watanzania hawako tayari kushiriki kwenye hoja au vitendo vitakavyopelekea uvunjifu wa amani kwa Taifa lao "Unapotaka kitu fulani ukaona umekosa kaa kimya, sasa wewe ukianza kuleta maneno maneno, sisi Watanzania tunaishi kwa amani, tunapendana, tunatoka kwenye eneo moja kwenda eneo jindine, hakuna Mtanzania yeyote aliye tayari kuharibu amani ya nchi" -Msama Msama ametoa kauli hiyo leo, Alhamisi Septemba 25.2025 alipokuwa Akizungumza na wanahabari kuhusiana na masuala mbalimbali yanayondelea nchini, ambapo pamoja na mambo mengine amedai kuwa kumekuwepo na wimbi linalotumia majukwaa ya mitandao ya kijamii kutoa kauli za uchochezi lengo likiwa ni kutengeneza chuki miongoni mwa Watanzania, jambo ambalo amesema halitofanikiwa Amesema kwa sasa, Watanzania wanaendelea kufuatilia kwa karibu kamp...

DOGO RED, WIZ DESIGNER KUTIKISA AFRIKA

Image
MSANII wa kizazi kipya mwenye makazi yake Atlanta, Marekani, Dogo Red, ametamba kutikisa Afrika Mashariki na video ya wimbo Vanessa aliowashirikisha wasanii wa Burundi Wiz Designer na Rich Forever. Dogo Red ni miongoni mwa wasanii wachache wapambanaji waliotokea Afrika Mashariki wanaoendelea kufanya muziki ughaibuni kwa mafanikio na Ijumaa hii anaachia kolabo hiyo. Akizungumzia kolabo hiyo Dogo Red ambaye ni bosi wa Wapamba Classic , amesema audio ya wimbo huo ilipokewa kwa kishindo na mashabiki katika mitandao mbalimbali ya kusikiliza muziki duniani na kiu yao sasa ni kuona video ya Vanessa ikitoka. "Nimejibu kiu ya mashabiki wa Dogo Red kwa kuachia hii video, nitaiachia Ijumaa hii kwenye chaneli yangu ya YouTube hivyo mashabiki zangu na wale wa Wiz Designer na Rich Forever tutakata kiu yao ya muda mrefu," amesema Dogo Red. @@@

STEVE NYERERE ATOA TATHIMINI SIKU 24 ZA KAMPEMI, AMKANDA POLEPOLE

Image
STEVE NYERERE ATOA TATHIMINI SIKU 24 ZA KAMPEMI, AMKANDA POLEPOLE Msaniii wa filamu na Mwenyekiti wa Mama Ongea na Mwanao Steve Nyerere ametoa tathimini yake ya hali ya kisiasa ikiwa ni siku 24 toka kipenga cha kampeni za uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uanze August 28, 2025. Katika tathimini yake amedai vyama vingi vya upinzani havijaonyesha umwamba wao, tofuati na CCM ambao wameonekana kukubalika katika maeneo mengi kutokana na mikutano yao kuvutia maelfu ya watu. Kwa upande mwingine akosoa vikali taarifa mbalimbali ambazo amekuwa akizitoa aliyekuwa Balozi wa Cuba na kada wa CCM kuhusu serikali yake ambayo ameitumia kwa miaka mingi. Steve amedai Polepole kwa sasa ni kama mchekeshaji kwani toka aanze kutoa matamko yake amekuwa akipuuzwa hali ambayo umemuondolea mvuto wake.

WANAFUNZI NI MUHIMU KUPATIWA ELIMU YA FEDHA

Image
Elimu ya fedha yatajwa kuwa muhimu kwa wanafunzi kukabiliana na changamoto. Na Brighitte WADAU wa elimu na maendeleo ya vijana wameeleza umuhimu wa wanafunzi kujifunza elimu ya fedha na ujasiriamali ili kuwajengea uwezo wa kujitegemea, kujikimu katika maisha ya shule na baada ya kuhitimu masomo yao. Wakizungumza katika Bonanza maalum la kuwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri katika kutekeleza miradi ya kibiashara kupitia Mradi wa Mshilo Club unaotekelezwa na taasisi ya Her Initiative, wadau hao wamesisitiza kuwa elimu ya fedha kwa wanafunzi ni njia bora ya kukabiliana na changamoto ya ajira. Mradi huo ulioanzishwa mwaka 2019, unalenga kuwawezesha wasichana kubaki shuleni kwa kuwapatia ujuzi wa elimu ya fedha, ujasiriamali na masoko, ili waweze kuwa na maarifa ya kujikimu katika maisha hata baada ya masomo. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Her Initiative, Lydia Charles amesema kuwa ujuzi huo huwasaidia wanafunzi kuelewa namna ya kusimamia fedha, kupanga matumizi ...

MAMA ONGEA NA MWANAO NA LAMATA VILLAGE WAPIGA HODI ZANZIBAR

Image
Wasanii wa mama ongea na Lamata Village wabisha hodi Zanzibar kumuunga mkono Dk. Samia na Dkt Mwinyi Wasanii wa Mama Ongea na Mwanao kwa kushirikiana na Lamata Village wameendelea kuonyesha mshikamanio wao wa kisiasa na kijamii baada ya kutangaza rasmi safari yao kuelekea Visiwani Zanzibar, wakimuunga mkono Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan na Dkt Mwinyi. Awali, wasanii hao walitoa shukrani za dhati kwa wananchi wa mikoa ya Mbeya, Njombe, Iringa, Singida, Tabora na Kigoma kwa kujitokeza kwa wingi katika kampeni za Dk. Samia, jambo walilolieleza kuwa ni ishara ya imani kubwa ya Watanzania kwa uongozi wake. Kwa mujibu wa wasanii hao, wameamua kujitoa kwa nguvu zote kuhakikisha Dk. Samia anaibuka kidedea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, ili aendeleze mazuri yaliyotekelezwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake. “Tunataka kuhakikisha mama anaendelea na safari yake ya kuwatumikia Watanzania. Ameyafanya makubwa ndani ya muda mfupi, hiv...

MSAMA:WANAOMTUKANA RAIS SAMIA NI WAHUNI

Image
WANAOMTUKANA RAIS SAMIA NI WAHUNI - MSAMA Mkurugenzi Mkuu wa Msama Promesheni Ndugu, Alex Msama amempongeza Mgombea wa Urais Kupitia Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dkt. Samia Suluhu Hassan Kwa kampeni zake alizozifanya Ndani ya Mwezi Mmoja bila kupumnzika huku akisema ameonyesha ukakamavu wa hali ya juu. Akizungumza na Waandishi wa Habari Kinondoni Jijini Dar es Salaam Msama amesema Mapokezi makubwa waliomuonyesha Wananchi Mikoani ni ishara yakuwa Atachaguliwa na kushinda kwa kishindo. Aidha Msama amewapa onyo wale wote wanaondelea kutoa lugha za matusi mitandaoni kuacha mara moja huku akiwasihi watanzania kuwapuuza watu hawa huku akidai wanatumika na mabeberu wasiokuwa na nia njema na Taifa la Tanzania huko nje ya nchi.

WASANII WAJITOKEZA KAZURAMIMBA KUMUHUNGA MKONO MAMA SAMIA

Image
KAZURAMIMBA tunasonga mbele!!!! Leo tupo hapa kuunga mkono kampeni za Mama Samia Suluhu Hassan kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025. Ni fahari yetu kuwa sehemu ya harakati hizi za maendeleo, tukisimama imara kuhakikisha tunaendeleza ilani ya CCM kwa mustakabali bora wa Taifa letu. Oktoba ni jukumu letu kutiki kwa Mama Samia! Huu ndio wakati wa kusimama bega kwa bega na kiongozi anayejali wananchi wake – Rais Samia Suluhu Hassan – ambaye ameahidi kuleta mabadiliko chanya, kuimarisha uchumi, na kufungua fursa zaidi kwa vijana. Kwa pamoja, tunashirikiana kuandika historia mpya ya maendeleo endelevu. Sauti yako ina thamani – tujitokeze kwa wingi Oktoba 29! @ccmtanzania @safariya_ccm @samia.app @samia_suluhu_hassan #MamaSamia2025 #CCM #Kazuramimba #MaendeleoTunayoYataka #OktobaNiyetu

WASANII WA MAMA ONGEA NA MWANAO NA LAMATA VILLAGE WAWA KIVUTIO KAMPENI ZA SAMIA

Image
Wasanii wa mama ongea na Lamata Village wawa kivutio kampeni za Dkt. Samia Wasanii kutoka makundi maarufu ya Mama Ongea na Mwanao pamoja na Lamata Village wameendelea kuwa kivutio kikubwa katika kampeni za Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutokana na ubunifu na kazi kubwa wanayoifanya mikoani. Makundi hayo yanayoongozwa na Steven Nyerere na Leah Lamata 'Lamata' yamekuwa chachu ya hamasa kila wanapofika kwenye mikutano ya kampeni, wakikonga nyoyo za wananchi kwa burudani na jumbe za mshikamano. Mashabiki wengi wamekuwa wakishangilia kwa nguvu kubwa kila mara wasanii hao wanapopanda jukwaani na kuhamasisha wananchi kumpigia kura Dkt. Samia, huku wakiahidi kumchagua ifikapo mwezi Oktoba. Kwa mujibu wa mashuhuda wa kampeni hizo, uwepo wa wasanii hao umeongeza mvuto na msisimko, hali inayochangia hamasa kubwa kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika kampeni na mchakato wa uchaguzi. Mwisho

BABA LEVO AFUNGUA KAMPENI KIGOMA MJINI

Image
Mgombea ubunge jimbo la Kigoma Mjini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Clayton Chipando (Baba Levo) amefungua Kampeni za Ubunge Jimbo la Kigoma mjini na kupokelewa na Maelfu katika viwanja vya Mwanga Community Center ambapo amesindikizwa na msanii ZUCHU, Dvoice na wengine wengi katika ufunguzi wa kampeni hizo…

KUSITISHWA KWA MCHAKATO WA UCHAGUZI WA KAMATI YA OLIMPIKI TANZANIA (TOC)

Image
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesitisha mchakato wa Uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) ambao ulipangwa ufanyike Oktoba 04, 2025 kutokana na kukataliwa kwa rufaa iliyowasilishwa na uongozi wa TOC kwa Waziri wa wizara hiyo dhidi ya maamuzi ya msajili wa Vyama vya Michezo. Imebainishwa uamuzi huo wa kusitisha mchakato wa uchaguzi huo umefanywa kwa mujibu wa kifungu cha 27(2) cha Sheria ya Baraza la Michezo la Taifa iliyofanyiwa marekebisho Na. 6 ya mwaka 1971, pamoja na kanuni za Usajili wa Vyama vya michezo za mwaka 1999 kanuni ya 11 (6) na (7) ambao ulifikishwa TOC kwa barua yenye Kumb. Na. BA.58/280/01/05 ya tarehe 30 Mei 2025 na barua yenye Kumb. Na. CBA.52/280/01/01 ya tarehe 03 Septemba 2025. Katika taarifa iliyotolewa leo Septemba 09, 2025 na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Hassan Mabuye imesema Mheshimiwa Waziri wa Wizara hiyo ametoa maelekezo hayo kwa kuwa TOC ilitangaza uchaguzi kwa kutumia Katiba ambayo sio halali na kutoa maa...

SERIKALI YASITISHA UCHAGUZI WA KAMATI YA OLIMPIKI

Image
SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesitisha rasmi mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) uliokuwa umepangwa kufanyika Oktoba 4, 2025. Uamuzi huo umetolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Professa Palamagamba Kabudi baada ya kubaini kuwa uongozi wa TOC ulitangaza uchaguzi kwa kutumia katiba isiyo halali. Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo iliyotolewa Dar es Salaam Leo na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano serikalini, Hassan Mabuye, Katiba inayotambuliwa kisheria na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) ni ile iliyoidhinishwa Novemba 26, 2020. Akitoa ufafanuzi, Mabuye, alisema Wizara imechukua hatua hiyo kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, uwajibikaji, utawala bora na utulivu katika sekta ya michezo. Miongoni mwa maelekezo yaliyotolewa na Waziri ni: Kusimamishwa mara moja kwa mchakato wa uchaguzi uliotangazwa na TOC. Kuanzishwa mara moja kwa mchakato mpya wa uchaguzi wa TOC kwa mujibu wa Katiba sahihi na tarat...

TAMTHILIA YA NICE TO MEET YOU MSIMU WA PILI KUANZA SEPTEMBA 15, 2025

Image
Tamthilia ‘Nice to Meet You’ Msimu wa pili ni kiboko yazidi kugusa Mioyo, ya mashabiki Wamama wengi wameeleza kupata faraja na hata kubarikiwa kupitia uigizaji wa msanii Hemed Suleiman ‘Hemed PHD’, anayejulikana kama Mchungaji Simon katika tamthilia maarufu ya Nice to Meet You. Akizungumza na SpotiLeo wakati wa uzinduzi wa msimu wa pili wa tamthilia hiyo, Hemed alisema kumekuwa na mrejesho mkubwa kutoka kwa mashabiki, hasa wanawake waliowahi kupitia changamoto zinazofanana na wahusika wa tamthilia hiyo. Katika msimu wa kwanza, Hemed aliigiza kama Simon, kijana mlokole aliyemsaidia mwanamke aliyejipatia kipato kupitia biashara ya kujiuza na kumrejesha katika njia ya imani. Swali linalobaki kwa mashabiki ni iwapo Simon ataendelea kushikilia ulokole au kurudi katika mapenzi ya zamani alipokuwa mwanafunzi. Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mahudhui na Masoko wa Startimes, David Malisa, amesema:“Hii ni sehemu ya kusapoti kazi za wasanii wa nyumbani na kuhakikisha jamii inapata maudh...

HELLO CHINESE S2 LANGO LA KIMATAIFA LA UTADUNI WA KICHINA

Image
Lango la Kimataifa la Utamaduni wa Kichina Kwa kuangalia wigo na upana wa mawasiliano ya kiutamaduni, kipindi cha “Hello Chinese” kimevuka mipaka ya kijiografia na lugha, na kuufanya utamaduni wa Kichina kufika nje ya mipaka na hatimae kuufikia ulimwengu. Msimu huu kipindi hiki kimeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Kituo cha Elimu na Ushirikiano wa Lugha (Wizara ya Elimu ya Jamhuri ya Watu wa China) na StarTimes. Kipindi hiki kinawapa fursa watu kutoka nchi na tamaduni mbalimbali nafasi ya kuwasiliana na kuelewa utamaduni wa Kichina, hivyo kimepelekea kupanua kwa kiasi kikubwa wigo wa usambazaji wake na kuuruhusu ulimwengu kuona China yenye taswira mbalimbali na yenye nguvu na uhai. Kufungua siri za kujifunza KichinaIdara ya "Usomaji na Uandishi wa Kichina" imeandaa njia za kujifunza kulingana na hatua ya kila mwanafunzi. Kipindi hiki cha “Hello Chinese” kinawaongoza wanafunzi hatua kwa hatua—kujifunza matamshi ya herufi, mikato yake, na hatimae kuunda senten...

JKCI YASHEREKEA MIAKA KUMI NA KUOKOA MABILIONI KATIKA MATIBABU YA MOYO

Image
Na Brighitte DAR ES SALAAM:TAASISI ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) tangu kuanzishwa mwaka 2015 imeokoa maisha ya watu zaidi ya milioni moja na kuokoa fedha kiasi cha Sh bilioni 172 ambazo zilikuwa zinatumika kupeleka wagonjwa wa moyo nje ya nchi. Akizungumza katika hafla ya kuadhimisha miaka 10 ya utoaji wa huduma za matibabu ya moyo katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi wa JKCI ,Dk Peter Kisenge amesema wanategemea kuokoa maisha ya watu wengi zaidi miaka ijayo hasa katika wakati huu ambao wanajikita katika matumizi ya akili mnembe. Dk Kisenge amesema katika miaka 10 wamefanya maendeleo makubwa hata hivyo bado wanaendelea kupanua huduma za moyo nchi kwa kujenga hospitali ya moyo ya watoto yenye vitanda 100 katika eneo la Mloganzila jijini Dar es Salaam. "Kwa sasa JKCI siyo tu ni Hospitali ya Tanzania bali ya Africa kwani wagonjwa kutoka nchi za Afrika na nje ya Afrika kama India, Uturuki, China, Ufaransa, Ujerumani, wanatibiwa h...