ASILIMIA 39.5 YA WANAWAKE WAATHIRIKA WA UKATILI; SERIKALI YATAHADHARISHA HATARI YA UKATILI WA KIDIJITALI
DAR ES SALAAM: Serikali imesema ukatili wa kijinsia unaendelea kuwa moja ya changamoto kubwa za haki za binadamu nchini, huku takwimu za kitaifa zikionesha kuwa asilimia 39.5 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49 wamewahi kukumbwa na ukatili wa aina mbalimbali, ikiwemo wa kimwili, kihisia na kingono kutoka kwa wenza wao. Aidha, wadau wameitaka jamii kuimarisha usalama wa kidijitali na kushughulikia ukatili wa kijinsia unaowezeshwa na teknolojia (TFGBV), ili kuruhusu wanawake na wasichana kushiriki kikamilifu katika elimu, fursa za kiuchumi, uongozi na maisha ya kiraia. Akizungumza jijini Dar es Salaam katika mkutano wa kitaifa kuhusu viashiria vya ukatili wa kijinsia vinavyofanyika kupitia teknolojia (TFGBV), Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watu wenye Ulemavu Zanzibar, Abeda Rashid Abdallah, amesema kuwa tatizo hilo linaongezeka kwa kasi na linahitaji hatua za haraka. Mkutano huo umeandaliwa na Shirika la Kimataifa la Idadi ya Watu ...