Posts

Showing posts from February, 2024

LADY IN RED KUCHANGIA WATOTO WENYE MATATIZO YA MOYO

Image
 Jukwaa la Mitindo la kuonyesha mavazi nchini Tanzania Lady in Red limekuja kivingine ni usiku wa kuonyesha mavazi yatakayo saidia watoto wenye matatizo ya moyo katika Taasisi ya Jakaya Kikwete. Onyesho hilo linalotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii February 17 katika ukumbi wa Were house uliopo jijini Dar es Salaam. Akizungumza na Habari leo Mwandaaji wa jukwaa la Lady in Red, Kampuni ya Hudo Domingo, Mary Fernandes amesema kuwa wamefanya mchujo wa wanamitindo (model Casting) walikuwa zaidi ya 200 wamepatikana 23 watakaopanda kwenye jukwaa hilo. "Kama kawaida yetu kila mwaka tunaangalia wapi tukapeleke kusaidia wenye uhitaji, mwaka huu tumelenga kuwasaidia watoto wenye matatizo ya moyo katika Taasisi ya Jakaya Kikwete waliopata matibabu na bado hawajalipia tutawalipia."amesema Mary Amesema gharama za matibatu ni kuanzia laki nane na kuendelea hivyo kwenye onyesho hilo wataingia na kiingilio VIP 50000 na kawaida elfu 30000 kitakachosaidia kuchangia matibabu ya watoto wen...

TAKUKURU IMESIMAMISHA KITUO CHA MAFUTA

Image
  Taasisi ya kuzuia na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Temeke imesimamisha ujenzi wa kituo cha mafuta uliokuwa unaendelea katika kiwanja namba P.18435 eneo la mbagala manispaa ya Temeke Dar es salaam  Hayo yamejiri leo Februari 5,Jijini dar es Salaam wakati Kaimu mkuu wa Takukuru Manispaa ya Temeke Euginius Hazina mwisho akizungumza na waandishi wa habari  kuhusu programu ya Takukuru rafiki ya kutatua kero ya ujenzi wa kituo cha mafuta kilichojengwa kinyume na utaratibu  Aidha, Hazina mwisho ameeleza uchunguzi wa kina kuhusu kutolewa kwa kibali hiko cha ujenzi ulibaini kwamba wapo baadhi ya watumishi wachache wasiowadalifu wa wizara ya Ardhi walikula njama na kufanikisha upitishaji wa kibali cha ujenzi kinyume na sheria  Pia,Hazina mwisho amesema wanaendelea kukamilisha uchunguzi ili wote waliohusika waweze kufikishwa mahakamani kwa makosa ya kughushi,Kula njama na matumizi mabaya ya ofisi "Tunaendelea kukamilisha uchunguzi ili wote waliohusika waweze kufikishwa mahak...

WANAUME TEMEKE RUSKA KUSHUHUDIA KWA MACHO WAKE ZAO AKIJIFUNGUA

Image
Hospitali ya Rufaa Mkoa Temeke (TRRH) imeanza rasmi kutoa huduma ya kujifungua ukiwa na msaidizi yaani mama, mume, mpenzi au ndugu na kuruhusu mama anayejifungua kuchagua muuguzi anayemtaka kama muongozo mpya wa chati uchungu unavyosema. Maboresho hayo yamefanywa ili kumwezesha mama mjamzito kupata huduma bora zaidi na kuwa karibu na msaidizi wake pamoja na kuzingatia utu na heshima kwa mama mjamzito. Hassan Mwauta mkazi wa Chamazi ambaye ni mume wa mmoja wa wajawazito waliotumia huduma hiyo katika hospitali hiyo ameipongeza Serikali kwa maboresho hayo. “Nilimleta mke wangu kuja kujifungua katika hospitali ya Temeke, nilisikia kuna huduma ya mzazi kujifungua akiwa na mwenza wake na nilipofika nimejionea mwenyewe, nimeshangaa kwa kweli mazingira ni mazuri na huduma ni nzuri, unaweza kuingia na mjamzito wako ukakaa naye muda wowote unaotaka,” amesema Mwauta. Naye Ofisa Mkunga katika hospitali hiyo, Shukrani William, amesema wodi ya kujifungulia kina mama imeboreshwa na kwamba huo ni moja...

MWANAFUNZI WA MIKA 15 AMPONZA RASHIDI APELEKWA JERA

Image
Mahakama ya Wilaya ya Temeke Dar es Salaam, imemuhukumu Racha Rashid (49) mkazi wa Tandika Mwembeyanga Manispaa ya Temeke, kwenda Jela maisha kwa kosa la kubaka binti wa miaka 15 mwanafunzi wa kidato cha pili. Imeelezwa Mahakamani hapo kuwa Racha alimbaka binti huyo kwa nyakati tofauti huku akimrubuni kwa kumpa pesa. Madili ametoa hukumu hiyo ya kifungo cha Jela maisha baada ya kuridhishwa na ushahidi uliowasilishwa Mahakamani hapo.

MUHIMBILI KUPONYA VIDONDA KWA NJIA YA HEWA TIBA

Image
Waliokuwa na vidonda kwa muda mrefu wapona baada ya kupatiwa matibabu Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa njia ya hewa tiba yenye mgandamizo wa oksijeni.   Hospitali ya Taifa Muhimbili itaendelea kuongeza huduma za kibingwa bobezi ili kuendelea kuwahudumia watu wengi zaidi ndani na nje ya nchi hatua itakayo endeleza kuchochea utalii tiba hapa nchini. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji Muhimbili Dkt. Rachel Mhaville wakati akizunguza na waandishi wa habari kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Prof. Mohamed Janabi, kuhusu huduma ya matibabu kwa njia ya hewa tiba yenye mgandamizo wa oksijeni (Hyperbaric Medicine Treatment), ambapo wanufaika wa huduma hiyo wamepata fursa ya kutoa ushuhuda juu ya matibabu waliyoyapata na afya zao kuimarika. Dkt. Mhaville amesema MNH ni hospitali ya kwanza ya Umma nchini na katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kutoa huduma hiyo na kwamba imekua na matokeo mazuri. “Leo tuna mashuhuda wawili ambao walikuwa na vidonda kwenye miguu yao kwa miak...

YANGA KUZINDUA JENGO LA KISASA KATIKA KUTIMIZA MIAKA 89l

Image
Klabu ya soka Young Afrika 'Yanga' imetimiza miaka 89 kuzindua jengo lao la kisasa jumatano katika kusherekea kuadhimisha kwake tangu mwaka 1935. Akizungumza Afisa habari na mawasiliano wa klabu ya Yanga Ali Kamwe amesema kuwa timu hiyo imeanza rasmi wiki ya kuadhimisha ukumbusho wa kuanzishwa na klabu hiyo inayotimiza miaka 89 tangu kunzishwa kwake 1935. Pamoja na mengi aliyotaja, Kamwe mamesema kawa watazindua jengo la makao makuu ya kisasa ya timu hiyo yaliyopo mitaa ya twiga na jangwani jijini Dar es salaam. “Leo rasmi tumeingia kwenye wiki ya anniversary ya miaka 89 ya Klabu hii kubwa Tanzania, kuelekea kilele cha Birthday ya Young Africans SC tarehe 11 mwezi huu wa pili, safari hii tuna mambo makubwa. Hii ni wiki yetu wenyewe” "Kesho Young Africans SC tutakwenda kusaini mkataba na Hospitali kubwa sana duniani, ikiwa na lengo la kumnufaisha shabiki wetu kwenye masuala yanayohusu afya yao. Klabu kubwa lazima iwaze kwa ukubwa namna gani Mwanachama wake atanufaika na Kla...

ALI KIBA NA NANDY WAACHIA DAH!

Image
Msanii wa Bongo fleva nchini Ali Kiba maarufu kama 'King Kiba' pamoja na mrembo wa kiwanda cha muziki Faustina Mfinanga, 'Nandy' wameachia wimbo wa Dah! Akizungumza wakati wa kuachia wimbo huo Nandy amesema ameona King Kiba ndie anae fiti kufanyanae kolabo hiyo. Pia King Kiba ameongeza kuwa Nandy alimtafuta na kumwambia kuwa wanaweza kufanya pamoja remix ya wimbo wa Dah

KAMPUNI YA AZAM YAZINDUA MFUMO WA KUCHUKUA TAMTHILIA

Image
K AMPUNI ya Azam Media imetambulisha mfumo mpya wa upokeaji wa kazi za tamthilia ya kitanzania zinazoruka kwenye Chaneli ya Sinema Zetu kuepuka wizi wa kazi za Sanaa. Akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam, msimamizi Mkuu wa Chaneli ya Sinema Zetu, Sophia Mgaza wakati wa uzinduzi wa mfumo huo mpya amesema kuwa uzalishaji wa tamthia  hiyo umezingatia mahitaji ya soko kwani wametumia vifaa vya uzalishaji wa kisasa na ubora wa hali ya juu,” amesema Mgaza. Amesema awalinilikuwa unapeleka demo kwanza kwa sasa hali imekuwa nitofauti unatakiwa kuingia mtandaoni kujisajili na kujaza fomu na kuweka mikataba mbalimbali ikiwemo mwandishi wa stori vibali vya Cosota,. Ameongeza kuwa waandaaji wapya wanaongia na kazi zao za sanaa zinazoruka kwenye chaneli hiyo  kuhakikisha wanasimamia ubora wa kazi ili wasije kutoa sababu kwa watu wa pembeni kuwanyooshea vidole na kusema kuwa ilikuwa ni nguvu ya soda tu,” amesema Mgaza.

JOH MAKINI ATUPA DONGO GIZANI

Image
Nini kinaendelea.? Joh Makin kamlenga nani kwenye hiii.? Ameandika… “Hii tasnia yetu bana kuna vitu vinafikirisha sana sometimes kufundishana uoga kwiingi mtu anakubali kushiriki kwenye wimbo kiroho safi unapofika wakati wa kushiriki promo kwa faida ya pande zote unakuta mtu kawekewa masharti magumu kama utajiri wa kishirikina!! #Formula”  Mpaka sasa ukipta kwenye page ya wasanii walioshirikishwa wimbo wa Formula na Joh Makini, msanii Jay Melody hajapost chochote kuhusu wimbo huo… Huku Bien akiwa am Esha post siku tano nyuma

ZANZIBAR INA AMANI, UMOJA, MSHIKAMANO NA UTULIVU

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar ina amani, umoja, mshikamano na utulivu pamoja na kuendelea shughuli za kimaendeleo na ibada.  Rais Dk. Mwinyi amesema hayo akizungumza alipojumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika  ibada ya sala ya Ijumaa na kufungua Ijitimai ya Kimataifa Tabligh Markaz Magome ya siku tatu Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba tarehe: 02 Februari 2024. Aidha Rais Dk.Mwinyi amewataka waumini kuendelea kumuomba Mwenyezi Mungu kudumisha amani, upendo, umoja na mshikamano. Halikadhalika Rais Dk.Mwinyi ametoa wito kwa waumini kuwafundisha watoto elimu ya dini ili wawe na hofu ya Mwenyezi Mungu kwa kujiepusha na matumizi ya madawa ya kulevya, wizi, ubadhirifu wa mali za umma na vitendo vya udhalilishaji . Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi ameipongeza Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar kwa kuratibu vizuri shughuli za dini  kwa utulivu, amani na mshikamano.

MAJALIWA AMWAKILISHA RAIS SAMIA KWENYE MKUTANO WA DHARURA WA SADC

Image
  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano wa dharura wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika kwa njia ya mtandao.   Mkutano huo uliofunguliwa na Rais wa Angola, Joao Manuel Lourenco ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, ulikuwa na ajenda moja tu ya kujadili kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu katika ukanda wa SADC.   Akizungumza kutoka ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma leo (Ijumaa, Februari 02, 2024), Waziri Mkuu Majaliwa amesema Tanzania inapendekeza kuwa ni vema Kanda ya SADC ikachukua hatua jumuishi kwa kuhusisha sekta zote mtambuka ikiwemo sekta za maji na mipango miji ili kuleta suluhisho la kudumu la kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu na magonjwa mengine ya mlipuko.   “Hii ni kwa kuzingatia kuwa jamii kwa ujumla na kila mwananchi ana jukumu la kuchukua tahadhari kwa kuhakikisha anazingatia kanuni za usafi (WASH) kwa manufaa binafsi, jamii na ukanda mzima.”   “...

AZAM YAJA NA TOBOA TOBO

Image
KAMPUNI ya Azam Media imetambulisha tamthilia ya kitanzania inazofahamika kama Toboa tobo ambayo imebeba simulizi na kuleta mapinduzi ya tasnia ya tamthilia nchini itakayoanza Februari 9 mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam, msimamizi Mkuu wa Chaneli ya Sinema Zetu, Sophia Mgaza amesema kuwa uzalishaji wa tamthia  hiyo umezingatia mahitaji ya soko kwani wametumia vifaa vya uzalishaji wa kisasa na ubora wa hali ya juu,” amesema Mgaza. Ameongeza kuwa waandaaji wapya wanaongia na kazi zao za sanaa zinazoruka kwenye chaneli hiyo  kuhakikisha wanasimamia ubora wa kazi ili wasije kutoa sababu kwa watu wa pembeni kuwanyooshea vidole na kusema kuwa ilikuwa ni nguvu ya soda tu,” amesema Mgaza. Pia amesema tamthilia hiyo inachukua nafasi ya tamthilia ya Mtaa wa Kazamoyo itakayofikia tamati February 8, 2024 na Toboa tobo kuanza rasmi  February 9 2024 kuanzia Ijumaa hadi Jumapili saa moja na nusu. Kwa upande wake mwongozaji wa tamthilia ya Toboa tobo Ma...