ALAFA APATA UFADHILI WA KUSOMEA UHANDISI WA NDEGE
Arafa apata ufadhili wa kusomea Uhandisi wa Ndege ARAFA Mazige, msichana mwenye ndoto ya kuwa mhandisi wa injini za ndege, amepata ufadhili wa masomo kupitia taasisi ya UNI-AID AFRICA na atasoma Shahada ya Uhandisi wa Ndege Chuo Kikuu cha JAIN nchini India. Msichana huyo kutoka Mvomero mkoani Morogoro alipata msukumo kutoka kwa baba yake, Hashimu Mazige, ambaye ni mbunifu wa teknolojia licha ya kutosomea rasmi. Alishuhudia baba yake akifufua gari lililokuwa limeharibika kwa miaka mitatu, jambo lililomtia moyo kuamini kuwa kila kitu kinawezekana. Akizungumzia mafanikio yake, Arafa anawahamasisha wanafunzi wenzake wa kike kujituma kwa kufanya vizuri darasani na kutumia mitandao ya kijamii kutafuta fursa za kielimu. "Nitaendelea kujifunza zaidi ya yale yanayofundishwa darasani ili kuleta maendeleo ya kiteknolojia na kuwasaidia wengine kama mimi,"amesema. Baba yake Hashim Mazige amesema kila mtoto anaweza kufanikisha ndoto yake ikiwa atapewa mazingira sahihi. ...