Posts

Showing posts from August, 2025

STARTIMES YAZINDUA KAMPENI MPYA ZOTE NDANI.

Image
Startimes Yazindua Kampeni Mpya ya Zote Ndani, Yaja na Ofa Maalum kwa Watazamaji Na Brighitte Davis, DAR ES SALAAM Kampuni ya Startimes imezindua kampeni mpya iitwayo Zote Ndani, ikiwapa watazamaji ofa maalum kupitia vipindi mbalimbali vya burudani, michezo, tamthilia na vipindi vya watoto. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Meneja Masoko wa Startimes, David Malisa, alisema kampeni hiyo inaleta vipindi vya kipekee sambamba na michezo ya kimataifa itakayorushwa kupitia kisimbuzi cha Startimes. “Tumejipanga kuonesha mechi kali kutoka Ligi Kuu ya England, La Liga na Bundesliga kupitia kisimbuzi chetu cha familia,” amesema Malisa. Mbali na michezo, Startimes pia imetambulisha tamthilia mbili kubwa kutoka Uturuki ambazo zimetafsiriwa kwa Kiswahili, ikiwemo Shadel T na Sagado Hadel Queen. Kwa upande wake, Godfrey Lugalabamu maarufu kama ‘Mc Gara B’, amesema msimu mpya wa Hello Mr. Right utarejea na maudhui mapya yenye msisimko. “Nimekuwa sehemu ya Hello Mr. Right tangu...

BOLT YAMKABIDHI MSHINDI WA JUJU KIDA ZAWADI

Image
Bolt Tanzania Yamtangaza Mshindi wa Kwanza wa Shindano la Dance Challenge Kampuni inayoongoza barani Afrika katika huduma za usafiri kwa njia ya mtandaoni, Bolt Tanzania, imemtangaza Juju Kida kuwa mshindi wa kwanza wa shindano lake la Bolt TZ Dance Challenge, lililofanyika kuanzia Julai hadi tarehe 25 Agosti. Shindano hili lililojumuisha muziki, ngoma na tamaduni, limevutia mamia ya washiriki kutoka maeneo mbalimbali nchini, likidhihirisha ubunifu na ari ya vijana wa Kitanzania. Kampeni hii iliendeshwa kupitia wimbo wa asili uitwao “Safari ni Bolt”, uliotungwa mahsusi kuonesha roho ya harakati na mshikamano. Wataalamu maarufu wa uchezaji Angel Nyigu na Dogo Noma waliongoza shindano kwa kutoa miondoko ya mwanzo, ambayo washiriki waliiga na kuiboresha kwa mitindo yao binafsi. Juju Kida, ambaye awali alishinda TSh 300,000 katika shindano la ngoma lililoandaliwa na kampuni ya michezo ya kubashiri, ameibuka kidedea kwa umahiri wake wa kisanaa na ubunifu wa kitamaduni. K...

SHINDANO LA KARAOKE KUFANYIKA LEO DAR AMELL

Image
FINALI ya Shindano la Uimbaji wa Karaoke nchini Tanzania inatarajiwa kufanyika leo katika Ukumbi wa Amell, jijini Dar es Salaam. Akizungumza na Amonlin, Mkurugenzi Mtendaji wa Soul Event, Allen Henjewele maarufu kama Allensoul, amesema maandalizi yote muhimu yamekamilika na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Kedmon Mapana. Henjewele amesema shindano hilo limekuwa kivutio kikubwa kwa vijana wengi wenye vipaji vya uimbaji na limefungua fursa za kimataifa. “Washindi wawili bora kabisa watapata heshima ya kuiwakilisha Tanzania kwenye jukwaa kubwa la Karaoke World Championship litakalofanyika jijini Bangkok, Thailand, Novemba 3, 2025,” amesema Henjewele. Mwisho

CHAMELEONE ATOA TALAKA ADAI MALI NIZA WATOTO

Image
Mkongwe wa Mziki nchini Uganda Joseph Mayanja maarufu kama Jose Chameleone amevunja ukimya kuhusu mwenendo wa talaka yake na Mke wake Daniella Atim waliofunga ndoa miaka 17 iliyopita na kusisitiza kuwa ingawa amekubali mali zake kugawanywa lakini hakubaliani na kitendo cha kulazimishwa kusaini wosia. Kwa mujibu wa ripoti ya Vyombo vya Habari Nchini Uganda vya BigEye na Pulse Uganda, Chameleone amesema hayo wakati akiwa LIVE kupitia kurasa zake Mtandaoni na kuweka wazi kuwa mali wanazogombea na Mkewe ni mali za Watoto na sio zao binafsi. “Mambo tunayopigania ni ya Watoto sio yetu na hata Watoto watawaachia Watoto wao, acha kutengeneza hali ambayo hakuna" amesema Chameleone. Mchakato wa kugawanywa kwa mali zake umeanza kuonekana mapema baada ya Mke wake kufungua mashtaka Mahakamani kudai talaka mnamo mwezi Machi mwaka huu ambapo August 21 alikubali kutoa talaka kwa kile Mkewe alichokiita kutelekezwa. Chameleone mwenyewe amesema kuwa hana pingamizi la kusaini hati za kisheri...

JENI AHUKUMIWA KWA KULA NAULI YA EMMA

Image
Mahakama ya Mwanzo jijini Lagos nchini Nigeria, imemhukumu Mwanamke anayefahamika kwa jina la Jennifer kulipa faini ya ₦450,000 sawa na zaidi ya Shilingi laki 730,000 za Kitanzania baada ya kupatikana na hatia ya kupokea fedha kwa udanganyifu. Kwa mujibu wa kumbukumbu za Mahakama, Jennifer alipokea 30,000 sawa na Shilingi 490,000 kutoka kwa kijana aitwaye Emmanuel, aliyedai kumtumia fedha hizo kwa ajili ya nauli ya kumtembelea nyumbani kwake, hata hivyo, baada ya kupokea fedha hizo, Jennifer hakufika kama walivyokubaliana na baadaye akakata mawasiliano. Emmanuel aliwasilisha malalamiko mahakamani, akieleza kuwa kitendo hicho kilikuwa ni aina ya utapeli wa kifedha, baada ya kusikiliza ushahidi, mahakama iliamua kwamba hatua ya Jennifer ilikuwa ni udanganyifu na unyonyaji wa kifedha, hivyo kumlipa Emmanuel fidia kubwa zaidi ya kiasi alichotapeliwa awali. Hakimu aliyesikiliza shauri hilo alisisitiza kwamba visa vya utapeli wa nauli ya usafiri vimekuwa vikiongezeka na vinachukuliwa k...

NIMEWAHI KUDATE NA GIGY VICHOCHORONI

Image
Staa wa bongo fleva Abdul Kiba ameweka wazi kuwa aliwahi kutoka kimapenzi na Gify Stanford kipindi ambacho alikuwa hajulikani kabisa hapa mjini. "Ni kweli nimewahi kuwa na mahusiano na Gigy ila ni kitambo sana. Kipindi hicho gigy Money alikuwa bado mdogo sana, Nadhani kati ya kikundi chake chote cha wanaume maarufu alichowahi kudate nao mimi ndio wa kwanza kipindi yupo anaishi vichochoroni uko."- Amefunguka Abdul Kiba Ikumbukwe Gigy Money aliwahi kudai kupitia mitandao ya kijamii kuwa aliwahi kuwa na mahusiano na Abdul Kiba na Ali Kiba, Licha ya wawili hao kusita kuithibitisha ukweli huo nashukuru leo Abdul Kiba ameongelea hilo jambo.

AMBER: MBOSSO ALINIOKOA NISIBAKWE

Image
Mwanamitandao na Msanii wa Bongo fleva Lulu Eugene 'Amber Lulu' amefunguka na kudai Msanii mwenzake Mbosso Khan anayetamba na wimbo wa 'Pawa' alimsaidia alipotaka kubakwa miaka ya nyuma. Amber ameweka wazi kuwa miaka ya nyuma Mbosso alishawahi kumsaidia alipokuwa anataka kubakwa Lakini pia hajawahi kumwambia mtu yoyote. "Kuna watu waachaee tu mungu amewapa roho zao sio za kawaida nakumbuka bila mbosso leo katika maisha yangu ningekuwa na stori ya kibakwa😢na sijawaji kusikia popote mpaka leo nimeongea mwenyewe."- Amefunguka Mbosso Toa maoni yako je kuna rafiki yako alishawai kukusaidia kitu ukakuta kakutangaza kwa watu.

TBN YAWAKEMEA VIKALI 'MANABII WA MITANDAONI YATAKA WAWAJIBIKE KWA SHERIA

Image
VIKALI 'MANABII' WA MITANDAONI, YATAKA WAJIBIKE KWA SHERIA Mtandao wa Bloga Tanzania (TBN) umekemea vikali tabia inayoshamiri ya watu kujinadi kufanya utabiri kwa watu na taifa kupitia mitandao ya kijamii, ukisema vitendo hivyo vinakiuka Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi. Kauli hiyo imetolewa kama azimio katika kikao kazi cha mafunzo ya mabloga kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. Mabloga hao wameitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) kushirikiana kuwasaka na kuwachukulia hatua kali wale wote wanaohusika na vitendo hivyo. Katika kikao hicho, mabloga walibainisha kuwa kumeibuka kundi la watu wanaodai kuwa ni manabii na kutoa kauli zinazokiuka sheria za nchi na kuleta taharuki kuelekea uchaguzi. Walisisitiza kuwa baada ya kuchambua Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (Personal Data Protection Act), walibaini kwamba 'utabiri' wa namna hiyo unavuruga haki ya msingi ya faragha ya wahusika. Kwa mujibu w...

DIRECTOR P AIBUKA UPYA NA MET YOU, REE NDANI

Image
Director P aibuka upya na Met You, Ree anogesha Msanii wa kizazi kipya na mwandaaji wa filamu mwenye asili ya Zambia na Kongo anayeishi nchini Canada, Patrick Lupasa 'Director P', amesema ngoma yake mpya, Met You imezidi kupenya kwa mashabiki zake barani Afrika tofauti na matarajio yake. Director P, amesema wimbo huo uliotoka hivi karibuni akimshirikisha mwimbaji Ree mwenye asili ya Jamaica na Canada alitarajia utajipatia umaarufu ughaibuni peke yake lakini mashabiki wa Afrika wamevutiwa nao zaidi. Akizungumza na AMNEWSONLI, Director P amesema huo ni ujio wake mpya wenye maudhui ya mapenzi na sasa yupo kwenye maandalizi ya kufanya video ili aendelee kuwapa raha mashabiki zake. "Wimbo huu unahusu jinsi upendo unavyosikika unapozungumzwa kwa lugha nyingi, Ree alileta ladha ya Karibea kwenye kurekodi Met You, na mimi nimeleta ladha ya Afrika Mashariki jambo lililofanya wimbo uvutie mno hii ni zaidi ya hadithi ya mapenzi na muunganisho wa kitamaduni," ames...

HUYU SASA NDO NANDY AFRICAN PRINCESS WA BILlNASS

Image
Africa Princess, muziki wake, tuzo, ndoa na muziki wake kimataifa Faustina Mfinanga anayefahamika kwa jina la Nandy ni mtunzi mwimbaji na Mwigizaji kutoka nchini Tanzania. Alizaliwa 9 Novemba 1992 mjini Moshi mikoani Kilimanjaro. Nandy amejipatia umaarufu mkubwa katika muziki wa Bongo fleva kupitia uimbaji wake wa Afro Pop akijulikana kwa sauti yake ya kuvutia na uwezo wake kuwasilisha hisia kupitia nyimbo zake. Nandy alianza safari yake ya muziki akiwa mdogo, akiimba kwaya kanisani. Baadae alijiunga na bendi ya muziki ya B band ambapo alifanya Maonyesho pamoja na kuimba na msanii mkubwa Banana Zorro. Mwaka 2017 alishiriki katika shindano la uimbaji ya Tecno Own Stage, ambalo lilimpa nafasi ya kushiriki katika Coke Studio Afrikawaka huo huo. Kupitia jukwaa hilo, alionheza umaarufu wake na kuanza kushirikiana na wasanii mbalimbali wa Kimataifa. Msanii Bora wa kike Afrika Mashariki mwaka 2017/2020 Tuzo Nandy ameshinda tuzo kadhaa za muziki ukiwa ni pamoja na All Africa ...

lULU DIVA: NILIKUNYWA SUMU BAADA YA PICHA ZANGU KUVUJA MTANDAONI

Image
“Lulu Diva afunguka: Nilikunywa sumu baada ya picha zangu kuvuja mtandaoni” Muimbaji na muigizaji maarufu wa Bongo, Lulu Abas almaarufu Lulu Diva, ameamua kufunguka kwa mara ya kwanza kuhusu tukio la kusikitisha na la aibu lililomkumba—picha zake za utupu kusambazwa mitandaoni. Akizungumza akiwa mgeni katika kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM, Lulu ameeleza kuwa tukio hilo lilitokea baada ya mpenzi wake wa zamani, mwanaume mwenye umri wa zaidi ya miaka 50 aliyekuwa anaishi Uingereza, kuvujisha picha hizo kama njia ya kulipiza kisasi baada ya kuachwa. "Nilijua vijana wameshaniumiza sana, nikasema nijitulize kwa mtu mzima, kumbe naye ana matatizo ya kisaikolojia," amesema Lulu Diva kwa sauti ya kujiamini lakini yenye huzuni iliyofichika. Lulu amesema kuwa picha hizo zilichukuliwa wakati wa mawasiliano yao ya video call, kipindi ambacho alikuwa na imani kubwa na mpenzi wake huyo kiasi cha kuweza kuzungumza naye hata akiwa bafuni. Lakini mambo yalibadilika walipoacha...

BUSHOKE AMVISHA PETE MCHUMBA WAKE

Image
Msanii wa muziki wa Bongo Flava hapa nchini Bushoke Luta amemchumbia mpenzi wake na hivi karibuni pengine tutarajie mualiko wa ndoa kutoka kwao. Bushoke amethibitisha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo amepost picha akiwa na mchumba wake na kuandika “She said yes” akimaanisha “Amesema ndio” 💍 Hongera sana Bushokeofficial

TADEA WACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA URAIS NA MAKAMU WA RAIS

Image
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha Tanzania Democratic Alliance (TADEA), Georges Gabriel Bussungu. Mgombea huyo waaliambatana na Mgombea Mwenza, Mhe. Ali Makame Issa (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 11, 2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. (Picha na INEC).

TCRA YATOA RATIBA YA MAFUNZO KWA TBN KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Image
TCRA yatoa Ratiba ya mafunzo kwa TBN kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeandaa mafunzo maalumu kwa Mtandao wa Mabloga (TBN) kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Mafunzo haya yatafanyika Jumatatu, Agosti 11, 2025, katika Makao Makuu ya TCRA. Kwa mujibu wa taarifa kutoka TCRA mafunzo hayo yana lengo la kuwaandaa mabloga na wanahabari kwa ujumla ili waweze kuripoti habari za uchaguzi kwa weledi na uadilifu. Mada mbalimbali zitakazowasilishwa na wataalamu kutoka taasisi tofauti. Baadhi ya mada zitakazojadiliwa ni pamoja na Mwongozo wa Waandishi wa Habari katika Uandishi wa Habari za Uchaguzi, Kanuni za Utangazaji wa Uchaguzi kwa Vyama vya Siasa za Mwaka 2020, na uhusiano kati ya Waandishi wa Habari na Jeshi la Polisi katika kulinda usalama. Mada nyingi zitatoka Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, itakayozungumzia maadili na sheria kwa waandishi wa habari, mada kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii na Akili Bandia (AI) kuelekea uchaguzi ...

TAMWA WAZINDUA MRADI WA UFUGAJI NYUKI

Image
TAMWA yazindua mradi wa ufugaji wa nyuk CHAMA cha Wanawake Waandishi wa Habari Tanzania (TAMWA) kimeanzisha mradi mpya wa ufugaji wa nyuki katika kijiji cha Msufini, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani, kwa lengo la kukuza uchumi wa jamii na kulinda mazingira dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi. Akizungumza katika mafunzo maalum ya ufugaji wa nyuki kwa wanachama wa TAMWA, Mkurugenzi Mtendaji wa chama hicho, Dkt. Rose Reuben amesema mradi huo unalenga kuwezesha wakazi wa Msufini kupata chanzo mbadala cha mapato kwa njia endelevu, salama na rafiki kwa mazingira. “Tunatarajia kuwa na mizinga 200 ya nyuki katika awamu ya kwanza. Licha ya kuongeza kipato kwa familia, mradi huu utachochea uhifadhi wa mazingira kupitia matumizi ya nyuki katika misitu na bustani. Ni wakati sasa wa kuunganisha ajira, mazingira na afya ya jamii kwa njia moja,” amesema Dkt. Reuben. Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2023, Tanzania huzalisha tani 20 tu za asali kwa mwaka, kiwango ambacho hakitoshelezi...