DAR BIASHARA MASAA 24 KUZINDULIWA FEBRUARI 22
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amesema uzinduzi rasmi wa biashara kwa saa 24 utafanyika Februari 22, mwaka huu 2025, na utaanzia eneo la Ofisini za Mkuu wa Mkoa hadi Kariakoo kuwa na matukio tofauti tofauti. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Chalamila amesema ufanyaji biashara kwa saa 24 unalenga kuimarisha uchumi wa mkoa, kuongeza mapato ya serikali na kutoa fursa za ajira. "Ufunguzi huo utaanzia ofisini za Mkuu wa Mkoa hadi Kariakoo ambapo ndipo watafanya ufunguzi rasmi. Ameeleza kuwa maandalizi ya ufungaji wa kamera za CCTV na taa za barabarani yanaendelea ili kuhakikisha usalama wa raia na mali zao unadumishwa. “Tunahakikisha mkoa wetu wa Dar es Salaam unakuwa na mazingira bora ya kufanya biashara muda wote, na tayari tunashirikiana na viongozi wa halmashauri kuimarisha maeneo yanayofaa kwa biashara za masaa 24,” amesema Chalamila. "Tutahakikisha tunapanga vizuri maeneo ya chakula pamoja na vinywaji ili...