Posts

Showing posts from July, 2024

STARTIMES ZOTE NDANI KAZI KWENU MASHABIKI

Image
  KAMPUNI ya Startimes imesema itaendelea kuunga mkono Ligi ya Championship ili kuwapa nafasi vijana kuonesha vipaji na kujiuza kimataifa. Imesema inatarajia kuonesha Ligi kubwa za Ulaya zikiwemo La Liga ya Hispania, Ujerumani Bundesliga, Saudi Arabia, Carabao Cup na Copa Del Rey. Hayo yamesemwa Dar es Salaam leo na Mkurugenzi wa Masoko na Maudhui kutoka Startimes David Malisa kwenye uzinduzi wa kampeni mpya ya zote ndani. “Ligi zote kubwa zitakuwa Startimes, tunaanza nyumbani na Championship kisha kimataifa na hiyo yote tunataka mashabiki zetu waendelee kubaki na sisi kwa kulipia vifurushi kwa bei ndogo na kuona namna vijana mbalimbali wanavyofanya vizuri,”amesema. Meneja vipindi na Maudhui kutoka Tv3 Emmanuel Sikawa amesema michuano hiyo yote itaruka kupitia Tv3 na kuhimiza mashabiki wa soka na wadau mbalimbali kutobaki nyuma bali ni wakati sahihi kuona vipaji vya soka vya ndani na kimatifa. Amesema  wamekuwa wakifanya vizuri kuonesha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa migu...

TUSIWACHUKULIE POA MABEKI TATU

Image
Msanii wa Filamu nchini Jacqueline Wolper amewaomba wanawake kuwapenda wadada wanao wasaidia kazi na kulea watoto wao nyumbani. Jacqueline amesema wadada wa kazi nao  wanauwezo mzuri na ushauri katika mambo mbalimbali, kama wazo lake la kujenga nyumba lilitoka kwa dada yake wake wa kazi  "Mimi wazo la kujenga nyumba nililipata kwa dada wa kazi (house girl) wangu, nilikuwa namlipa mshahara kumbe alikuwa anatunza hadi siku aliyokuja kuniambia anashukuru kwa pesa nizokukuwa nikimlipa.  "Dada nashukuru kwa msaada wako mimi nimejenga nyumba kupitia mshahara wako" Hapo ndipo akili ikanijia kuwa kumbe hata mimi naweza kujenga nyumba kwa kusevu pesa kidogo kidogo"  "Tangu hapo nilianza kusevu pesa kwa ajili ya nyumba na hatimae nikafanikiwa kujenga nyumba kubwa, nzuri ambayo thamani yake huenda ni zaidi ya shilingi milioni 500 za Tanzania ingawa bado haijaisha vizuri."  Pia Jacquline amesema kuwa anamshukuru house girl wake kwa kumpa wazo nzuri.

SNURA AIKIMBIA TASNIA YA SANAA

Image
Msanii wa Muziki wa Bongo fleva na Bongo Movie Snura Mushi ametangaza kuacha na na tasnia ya sanaa kwa ujumla ameamua kumrudia Mungu wake. Snura amesema kuwa anajutia maisha haliyoyaishi akiwa msanii yaliokuwa mabaya yasiyompendeza Mwenyezi Mungu atamani hata kuwa mfano kwa mtu yoyote. "Mimi Snura Mushi kuanzia leo nikiwa na akiri yangu timamu natangaza kuacha muziki na kazi zote zinazo husiana na sanaa nisihusishwe. "Nimejitambua mimi ni mtoto wa kiislamu nimeamua kufanya yanayo mpendeza Mungu ibada na kumtumikia, niliamua kumrudia Mungu tangu miaka miwili iliyopita ndo mana uliona nipo kimya sijafanya chochote kinachohusiana na Sanaa."amesema Snura Snura amesema kuwa anaomba asihusishwe wala kupigiwa simu kuhusu kitu chochote kinacho husiana na sanaa wala hana mpango navyo tena. "Sitaki watu wapige nyimbo zangu zote na ikitokea siku nimefariki watu wasipost picha zangu za hovyo nilizowahi kupiga kwani najuta kwa kupiga picha hizo na sitaki watu wengine waige mfano...

TMDA :HAKUNA KIRUSI KINACHOKAA KWENYE DAWA HII

Image
MAMLAKA ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA) imekanusha kwa mara nyingine kuwa  hakuna virusi vinavyojulikana kwa jina la Machupo au  virusi vya aina yoyote haviwezi kuishi kwenye kidonge.  Awali taarifa ilisambaa katika mitandao ya kijamii ikisema dawa aina ya Paracetamol ambayo imeandikwa P 500 na  kudaiwa kubabua ngozi Taarifa hiyo ilisema "Dawa hiyo inadaiwa kuwa ni ‘’paracetamol mpya nyeupe sana na inayong'aa,madaktari  wanashauri kuwa ina virusi vya "Machupo", inayochukuliwa kuwa moja ya virusi  hatari zaidi ulimwenguni, na kiwango cha juu cha vifo. Aidha, Mtoa taarifa anaitaka jamii kuisambaza taarifa hii kwa kila mtu aliyeko katika orodha yake ya mawasiliano ili kuokoa maisha. ‘’Nimefanya  sehemu yangu, sasa ni zamu yako. Kumbuka kwamba Mungu huwasaidia wale wanaosaidia wengine. ‘’Sambaza kama ilivyopokelewa,"amesema mtoa taarifa huyo  Akitoa ufafanuzi kuhusu dawa hiyo katika taarifa yake Mkurugenziwa TMDA ,Adam Fimbo ameeleza kuwa, Taarifa hiyo i...

NANDY NDIO ALINIAMBIA NIVAE KITOVU NJE

Image
Msanii wa Bongo fleva nchini Yammy amesema kuwa anapovaa na kuacha kitovu wazi alishauriwa na Boss wake Faustina Mfinanga 'Nandy'  Yammy amesema kuwa awali alikuwa anashindwa kuvaa hivyo lakini siku zilivyozidi kwenda amejikuta amezoea. "Watu wasichokijua Boss wangu Nandy ndie aliyenishauri kuvaa hivyo na kuacha kitovu nje kwa sababu nina umbo zuri na bado umri wangu ni mdogo hivyo nikivaa napendeza." "Nandy hawezi kuvaa hivyo kwa sababu umri wake na wangu ni tofauti na ukizingatia yeye ameshakuwa mama anamtoto na  ameolewa lakini kipindi cha nyuma akiwa na umri kama wangu ameshavaa sana."amesema Yammy Pia Yammy ameweza kujizolea umaarufu zaidi tangu alipoanza kuvaa na kuacha kitovu nje hivyo ni sehemu ya kutembea na upepo huo anapotangaza kazi zake. Lakini pia msanii kama Ray C, Rachel Kizunguzungu pamoja na Mwanadada Judith Wambura Lady Jay Dee ni miongoni mwa wasanii walipokuwa wakiacha vitovu nje lakini umri ulivyosogea waliacha.

SHILOLE MUUZA CHAKULA ESHA NI MPISHI

Image
Msanii wa Filamu nchini Esha Buheti ameweka bayana kuwa Zuwena Mohammed 'Shilole' ni muuza Chakula lakini yeye ni mapishi. Esha Buheti amesema kuwa Shilole anaivisha chakula ili watu wale lakini yeye ni mpishi anayepika chakula kikaiva na watu Wakala. "Mimi situmii karanga acha yeye aweke karanga kwenye tembele  wali karanga kila chakula, kwa kupika Shilole hanipati hata kidogo, aache kuivisha chakula ajifunze upishi apike chakula kinachoeleweka. "Lisemwalo lipo kama halipo laja akubali tu kwenye upishi hayupo ila, hii imekuja kutokana na kwenye ubaya wema ulikuwepo, ni kawaida sana rafiki kuwa adui ni rahisi kuliko adui kuwa rafiki." Esha amesema "acha watu wamjaze wee na yeye anajaa  nafutahia tu anachofanya sina muda wa kugombana yeye anapenda kidogo tupigane me napenda amani Shilole acha roho mbaya." Aidha amesema kuwa "Zuwena ameshazoea kupiga wanaume siwezi kupigana aende akapigane na mwiliwake huko apungue asiwaze kupigana na Esha akishidwa ...

DKT. BITEKO AWAKEMEA WATUMISHI WANAOKWAMISHA WAFANYABISHARA

Image
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka watumishi Serikalini kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na misingi ya utoaji wa huduma ili kuleta matokeo Chanya na sio kuwakwamisha watu wanohitaji huduma. Dkt. Biteko ametoa agizo hilo (Julai 30,2024) wakati akizindua Sera Taifa ya Biashara katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka Serikalini na sekta binafsi. Amesema katika baadhi ya ofisi kuna watu mahiri wa kuandaa maandiko lakini utekelezaji wa majukumu yao hauna uhalisia na hauendani na nyaraka walizoziandaa na hivyo nyaraka hizo kubaki kwenye makablasha. “ Tunaweza kuwa wazuri sana wa kuandika kutoa matamko na kutoa ahadi lakini hali halisi haibadiliki, Hakuna faida ya kuwa na afisa anayejipanga kumkwamisha mfanyabiashara ili tu aitwe bosi, Tunatakiwa kuwa na nyaraka inayotuunganisha wote vinginevyo sera hii itabaki kuwa kitabu cha hadithi kwenye kabati,” Amesema Dkt.Biteko Amewahimiza watumishi serikalini kuw...

GRAND GALA DANCE KUFANYIKA AGOSTI 30 THE SUPER DOME

Image
  Msimu wa tatu wa Grand Gala Dance kufanyika unatarajia kufanyika 30 Agosti 2024 katika ukumbi wa The Super Dome Masaki uliopo jijini Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Mkurugenzi wa Chocolate Princess na Muandaaji Mboni Masimba amesema kuwa Grand Gala Dance itapambwa na burudani kutoka kwa Bendi nne ikiwemo FM Academia. "Usiku wa Grand Gala Dance imeanzishwa nahususi kwa ajili ya kumuhenzi Rais wa Awamu ya kwanza wa Jamhuri wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere na utakuwa na burudani kutoka kwa Bendi ya  FM Academia, Christian Bella, Twanga Peteta na Tukuyu Sound. "Zitakazo konga nyoyo za watanzania  zitatumbuiza mubashara ikiwa ni kumbukizi ya kumuhenzi Baba wa Taifa kwa makubwa aliyoyafanya katika Taifa letu la Tanzania. Naye Pancho Mwamba amesema kuwa wananchi watarajie muziki mzuri kutoka kwa Bendi ya AF Academia kumbuka sio mashindano Bali ni muziki mzuri kutoka kwao. Kwa upande wake Christian Bella amesema kuwa hadi tarehe 30 atakuwa tayar...

DSTV TUMEKUELEWA WASHUSHA VINGAMUZI

Image
Kampuni ya MultiChoice Tanzania DStv imesema itaanza kuonesha tamthilia za kigeni kwa Lugha ya Kiswahili kuanzia Julai 20 mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa Masoko wa DStv Tanzania Baraka Shelukindo amesema sababu kubwa ya kuzitafsiri kwa Lugha ya Kiswahili ni kuhakikisha inawafikia Mamilioni ya wateja wake ukanda wa Afrika Mashabiki. "Kupitia kampeni mpya ya Tumekusikiliza tunataka kuwafikia wateja wetu kwa burudani mbalimbali na sasa tunakuja na tamthilia za Kituruki kwa Lugha ya Kiswahili cha kufanya kwa wateja wetu ni kulipia vifurushi,"amesema. Amesema "kila mtu hivi sasa lazima awe wa kimataifa kwa kumiliki DStv kirahisi na kuona mambo yote kama Mpira, Filamu na tamthilia mbalimbali,"amesema Shelukindo Pia amesema kuwa 29 Julai kuanza itaanza kuruka tamthilia ya kigeni inayoitwa The Boy pia kutakuwa na thamthilia ya Kiswahili inayoitwa Yolanda itaanza kuruka rasmi katika Magic Bongo.

HARMONIZE APATA DILI LA BUKUA MILIONI

Image
  Msanii wa Bongo fleva nchini Rajab Abdul 'Harmonize' amepata Dili la Mchezo wa kubashiri unaojulikana kama Bukua Mamilioni. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi rasmi wa Mchezo huo Harmonize amesema kuwa  hii itasaidia watanzania kujishindia vitu mbali mbali. "Ninafasi ya watanzania kujipatia ajira kupitia kampuni hii kwa kutumia pikipiki ambazo zitakuwa zikutolewa kila Ijumaa kwa mshindi atakaye shinda. "Lakini zawadi hizo hazitakuwa kwa washindi wa Dar tu peke yao tutatoa hata kwa watakaoshinda mikoani nitahakikisha nawakabizi mwenyewe kwa mikono yangu zawadi yoyote atakayoshinda mshindi Mkoa wowote hule."amesema Harmonize

THE CHINESE BASED SHUDAO INVESTMENT GROUP (SDIG)

Image
The Chinese based enterprise, Shudao Investment Group (SDIG), has promised to cooperate with the government to enhance high-level exchanges by deepening cooperation further in various fields including infrastructure. Speaking to reporters at the ongoing 46th Dar es Salaam International Trade Fair (DITF) in Dar es Salaam yesterday, SDIG managing director Hamid Idrissa Hamid mentioned other areas that the company eyes cooperation with the government are mining and clean energy.  “Specifically, as an sincere old friend to Tanzania, SDIG with the Tanzania government and companies have been successful in cooperation in transportation and has witnessed progress since 2006. We are vowing to enhance high-level exchanges between SDIG and Tanzania, and deepen cooperation further in various fields not only infrastructure, but also mining, clean energy and so on. SDIG hopes to bring concrete benefits to Tanzania people and joins hands with African friends to jointly achieve a win-win future,” ...

VIJANA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA KILIMO

Image
VIJANA watakiwa kuchangamkia fursa zilizopo katika miradi ya kilimo, ili kujitengenezea ajira ya kudumu na  kuachana na kusubiri kuajiriwa. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli katika kongamano la vijana wanaojihusisha na kilimo nchini, lililoandaliwa na Shirika la Mageuzi ya Kijana Tanzania (AGRA) kupitia mradi wa Building a Better Tomorrow (BBT). “Wizara ya kilimo kwa kushirikiana na asasi zisizo za kiserikali tumeandaa mpango maalumu kuhakikisha vijana wanajitengenezea ajira ya kudumu kupitia kilimo, na sasa hivi International Forums zote zitahusisha vijana ambapo vijana watakuwa wakisafiri nje ya nchi, ili wakajifunze namna ya kuwekeza kwenye kilimo. “Nitoe wito kwa vijana jiajirini kwenye kilimo, kinalipa na sasa hivi baadhi ya mashirika kutoka mataifa ya nje yanataka kuleta fund kwa ajili ya vijana wa kitanzania wanaojihusisha na kilimo,”amesema Mweli. Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa AGRA, Vianey Rweyendela amesema kukua kwa uchumi wa Tanzania k...

WATANZANIA WATAKIWA KULINDA VIUMBE VYA BAHARINI

Image
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati,  Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kulinda viumbe vya baharini na kuhifadhi mazingira ya bahari kwa ajili ya vizazi vilivyopo na vizazi vijavyo. Dkt. Biteko amesema hayo leo  Julai 4, 2024 wakati akifungua kongamano la Tatu la Uchumi wa Buluu mwaka 2024 yenye kaulimbiu: Kuunganisha Usalama Baharini, Utunzaji wa Mazingira na Maendeleo ya Teknolojia kwa ajili ya Ukuzaji wa Uchumi wa Buluu "Tunapofanya majadiliano leo, tujikite kwenye kanuni uendelevu, usawa na uvumbuzi ili hatimaye kongamano hili liwe mwanga unaotuongoza kwenye uchumi wa buluu unaoinua jamii zetu, ninawasihi kila mmoja wenu ashiriki kikamilifu ili tuweze kupata matokeo chanya ya kongamano hili," amesema Dkt. Biteko. Amesema uchumi wa buluu unatambuliwa kama mchangiaji mkubwa wa maendeleo endelevu ambapo jamii hutumia rasilimali za bahari kwa njia ambayo ni endelevu na kwa kiasi kikubwa huzingatia uhifadhi wa mazingira. Pia, uchumi wa buluu huchochea uvumbuzi wa fursa...

RIBA YA BANKI KUU BADO ASILIMIA 6

Image
Kamati ya Sera ya Fedha (MPC)ya Bodi ya Wakurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania, (BOT)  imeamua Riba ya Benki Kuu (CBR) itaendelea kuwa asilimia 6 kwa robo mwaka unaoishia Septemba 2024. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Naibu Gavana Kayanda Kayandabila amesema Uamuzi huu umefikiwa katika kikao cha Kamati kilichofanyika Julai 3,2024.  "Tathmini ya Kamati kuhusu mwelekeo wa uchumi na vihatarishi mbalimbali  inaonesha kwamba,utekelezaji wa sera ya fedha kwa kipindi cha Januari hadiJuni2024 umefanikiwa kudhibit mfumuko wa beina kubaki chini ya lengo la asilimia 5. "Maamuzi ya Kamati pia yanazingatia mtazamo chanya wauchumi wa dunia, ambapo matarajio ni kuendelea  kupungua kwa mfumuko wa bei katika nchi nyingi, kuimarika kwa ukwasi katika masoko ya fedha duniani, na kushuka kwa beiza bidhaakatika soko la dunia.  Aidha, Kamatiinatarajia uchumi wa  ndanikuendelea kukua kwa kasi, sanjari na upatikanaji wa chakula chakutosha, na kupungua kwa kasi...

DM MALL NA MMG WASHUSHA MIZOGO USHINGWE WEWE

Image
Viwanda 25 vya China vimetua nchini kushiriki maonesho ya Sabasaba 2024 chini ya uratibu wa Kampuni za usafitishaji mizigo za Kitanzania za DM Mall na MMG Logistics. Akizungumza na habari leo  Mkurugenzi  wa kampuni hizo Hamid Idrissa Hamid alisema lengo la ujio wa kampuni hizo ni kuonesha bidhaa wanazozalisha, kutengeneza mtandao na wafanyabiashara wa Tanzania lakini pia, kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan za kuwavuta wawekezaji kutembelea nchini na kuona fursa zilizopo. Ametaja miongoni mwa viwanda vilivyokuja ni pamoja na vya nguo, vifaa vya majumbani, simu, solar, viatu, mitambo, vinywaji, Jenereta, magari, vyakula, bidhaa za urembo na bidhaa mbalimbali ambapo pia, watatumia maonesho hayo kuuza na kuonesha shughuli zao. "Lengo la kuwaleta hatutaki kikundi Cha watu kinufaike peke yao bali tunataka Mtanzania mmoja mmoja anufaike apate kitu kwa bei ndogo ili kuyavutia makampuni hayo kuwekeza nchini na hatimaye kufungua viwanda na  kutoa ajira nyingi  kw...