TMDA :HAKUNA KIRUSI KINACHOKAA KWENYE DAWA HII
MAMLAKA ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA) imekanusha kwa mara nyingine kuwa hakuna virusi vinavyojulikana kwa jina la Machupo au virusi vya aina yoyote haviwezi kuishi kwenye kidonge.
Awali taarifa ilisambaa katika mitandao ya kijamii ikisema dawa aina ya Paracetamol ambayo imeandikwa P 500 na
kudaiwa kubabua ngozi
Taarifa hiyo ilisema "Dawa hiyo inadaiwa kuwa ni ‘’paracetamol mpya nyeupe sana na inayong'aa,madaktari
wanashauri kuwa ina virusi vya "Machupo", inayochukuliwa kuwa moja ya virusi
hatari zaidi ulimwenguni, na kiwango cha juu cha vifo.
Aidha, Mtoa taarifa anaitaka jamii kuisambaza taarifa hii kwa kila mtu aliyeko katika orodha yake ya mawasiliano ili kuokoa maisha. ‘’Nimefanya
sehemu yangu, sasa ni zamu yako. Kumbuka kwamba Mungu huwasaidia wale wanaosaidia wengine. ‘’Sambaza kama ilivyopokelewa,"amesema mtoa taarifa huyo
Akitoa ufafanuzi kuhusu dawa hiyo katika taarifa yake Mkurugenziwa TMDA ,Adam Fimbo ameeleza kuwa, Taarifa hiyo imekuwa ikijirudia mara kwa mara na TMDA imekuwa ikitolea ufafanuzi
ikiwemo taarifa ya mnamo tarehe 10 Mei, 2023, juu ya dawa aina ya P-500®
(PARACETAMOL) ya Apex Laboratories Private Limited, Tamil Nadu, India
iliyodaiwa kuwa na virusi hivyo.
Amesema TMDA inapenda kuwahakishia wananchi kuwa inaendelea kutimiza wajibu wake wa
kulinda afya ya Jamii kwa kuhakikisha kuwa bidhaa tiba zinazotumika nchini ni zile
zenye kukidhi matakwa ya ubora, usalama na ufanisi.
Vilevile, Mamlaka inapenda kuwakumbusha wananchi umuhimu wa kupata ufafanuzi
kutoka kwenye mamlaka husika kabla ya kusambaza taarifa zinazoweza kuleta
taharuki kwenye Jamii.
Aidha, Wananchi wanaweza kupiga simu ya bila malipo: 0800110084 endapo wapatapo taarifa za mashaka kama hizo.

Comments
Post a Comment