KAJALA AFUNGUKA UKWELI KUHUSU LULU KUJITOA KUNDI lA BIG SIX
Kajala Afunguka: Ukweli wa Kuvunjika kwa Kundi la “Big Six” na Brighitter Msanii maarufu wa filamu nchini, Kajala Masanja, amefunguka na kuweka wazi ukweli kuhusu kuvunjika kwa kundi lao maarufu lililojulikana kama “Big Six”, lililowakutanisha wasanii wakubwa wa kike nchini. Akizungumza kuhusu kundi hilo, Kajala amesema ni kweli walikuwa wasanii sita waliounda umoja huo, ambao ulihusisha Wolper, Aunty Ezekiel, Wema Sepetu, Kajala Masanja, Irene Uwoya na Elizabeth Michael (Lulu). Kajala amesema mwanzo wa kuvunjika kwa kundi hilo ulianza pale Elizabeth Michael alipokuwa wa kwanza kujiondoa. Kwa mujibu wa Kajala, Elizabeth aliwaeleza wenzake kuwa alikuwa anatarajia kuingia katika maisha mapya ya familia. “Elizabeth alituambia kuwa hivi karibuni anatarajia kuitwa mama, hivyo alihitaji muda mwingi kuwa karibu na mume wake na watoto wake,” amesema Kajala. Baada ya maelezo hayo, Kajala anasema wanakundi walikubaliana kumpa nafasi Elizabeth Michael ili ajikite kwenye familia ya...