Posts

Showing posts from 2025

KAJALA AFUNGUKA UKWELI KUHUSU LULU KUJITOA KUNDI lA BIG SIX

Image
Kajala Afunguka: Ukweli wa Kuvunjika kwa Kundi la “Big Six” na Brighitter Msanii maarufu wa filamu nchini, Kajala Masanja, amefunguka na kuweka wazi ukweli kuhusu kuvunjika kwa kundi lao maarufu lililojulikana kama “Big Six”, lililowakutanisha wasanii wakubwa wa kike nchini. Akizungumza kuhusu kundi hilo, Kajala amesema ni kweli walikuwa wasanii sita waliounda umoja huo, ambao ulihusisha Wolper, Aunty Ezekiel, Wema Sepetu, Kajala Masanja, Irene Uwoya na Elizabeth Michael (Lulu). Kajala amesema mwanzo wa kuvunjika kwa kundi hilo ulianza pale Elizabeth Michael alipokuwa wa kwanza kujiondoa. Kwa mujibu wa Kajala, Elizabeth aliwaeleza wenzake kuwa alikuwa anatarajia kuingia katika maisha mapya ya familia. “Elizabeth alituambia kuwa hivi karibuni anatarajia kuitwa mama, hivyo alihitaji muda mwingi kuwa karibu na mume wake na watoto wake,” amesema Kajala. Baada ya maelezo hayo, Kajala anasema wanakundi walikubaliana kumpa nafasi Elizabeth Michael ili ajikite kwenye familia ya...

MWAKINYO KUWANIA HESHIMA YA TAIFA LEO WARE HOUSE

Image
BONDIA wa kimataifa Hassan Mwakinyo leo anaipeperusha bendera ya Tanzania katika pambano kubwa la Boxing on Boxing Day dhidi ya mpinzani wake kutoka Nigeria, Stanley Eribo, litakalofanyika Desemba 26, 2025, katika Ukumbi wa Warehouse, Masaki jijini Dar es Salaam. Mwakinyo, ambaye ameongoza zoezi la upimaji uzito pamoja na mabondia wengine, amesema yuko tayari kikamilifu kwa pambano hilo, akiahidi ushindi kwa Watanzania. Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Mwakinyo alisema amejiandaa kwa kiwango cha juu na yuko tayari kumpambana mpinzani wake kwa nguvu zote. “Nimejiandaa vizuri sana kwa pambano hili. Nimemuandaa mpinzani wangu kikamilifu na nawahakikishia Watanzania ushindi mkubwa. Nitaingia ulingoni kuipigania heshima ya taifa,” amesema Mwakinyo. Kwa upande wake, bondia wa Tanzania Hamadi Furahisha amesema maandalizi yake yamekamilika na yuko tayari kukabiliana na mpinzani wake kutoka Malawi, Hanock Phiri. “Najua ninampinzani mkali, lakini niko tayari kumpa pambano gumu ...

STARTIMES YAZINDUA AGLIMPSE OF CHINA MSIMU WA TANO

Image
StarTimes Yazindua “A Glimpse of China S5” Kuimarisha Uelewano kati ya China na Afrika KAMPUNI ya StarTimes imezindua rasmi msimu wa tano wa kipindi cha “A Glimpse of China”, mradi wa pamoja kati ya StarTimes na Idara ya Kimataifa ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), unaolenga kuimarisha mawasiliano, uelewano na ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2020, kipindi hicho kimekuwa chanzo muhimu cha taarifa kinachoelezea safari ya China katika maendeleo ya kisasa, kikitoa picha halisi ya mabadiliko ya kiuchumi, kijamii na kiteknolojia yanayoendelea nchini humo. Msimu wa tano unaangazia kwa kina mafanikio ya China katika ubunifu wa kiteknolojia, uhuishaji wa vijijini, ustawi wa wananchi pamoja na juhudi za uhifadhi wa mazingira. Maudhui hayo yanawasilishwa kupitia simulizi fupi, zenye mvuto na zinazolenga kuwafikia kwa urahisi watazamaji wa Afrika. Kwa mujibu wa waandaaji wake, mtindo huo wa uwasilishaji unawezesha watazamaji ...

MCHANGE: HATUWEZI KUUZA UHURU WETU KWA WAZUNGU

Image
Mwenyekiti wa Kituo cha Wanahabari Watetezi wa Rasilimali za Taifa (MECIRA), Habibu Mchange, amekemea kauli za baadhi ya viongozi wa kisiasa wanaodaiwa kutaka kuirudisha Tanzania katika mifumo ya kikoloni au ya utumwa mamboleo. Akizungumza leo Desemba 12, 2025, jijini Dar es Salaam, Mchange alisema kuwa kauli hizo zinahatarisha misingi ya uhuru wa nchi na maslahi mapana ya Watanzania. Ametoa msimamo huo wakati akijibu hoja za Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche, kufuatia tamko lililotolewa na chama hicho hivi karibuni. Mchange amesisitiza kuwa, kama sehemu ya jamii ya Watanzania, MECIRA inawakumbusha wanasiasa wote kwamba maslahi ya Taifa yanapaswa kupewa kipaumbele kuliko maslahi ya vyama vyao.

TANZANIA AND U.S. MOVE TO FINALISE MAJOR INVESTMENT AGREEMENTS

Image
Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania, today held talks with the Acting United States Ambassador to Tanzania, Andrew Lentz, at Chamwino State House to advance key areas of bilateral cooperation and reaffirm the shared commitment to a modern, mutually beneficial partnership. Ambassador Lentz—accompanied by the Counselor for Political and Economic Affairs—underscored Washington’s determination to reset the relationship and deepen economic, political, and security collaboration with Tanzania. “The United States is committed to a partnership based not on aid dependency but on shared prosperity,” Ambassador Lentz said. The discussions centred on ongoing negotiations involving major U.S.-linked strategic investments. Both sides acknowledged that talks on two flagship projects—the LNG Project and Tembo Nickel Project—are now in their final stages, pending formal signing. A third investment, the Mahenge Graphite Project, remains under acti...

TANZANIA NA MAREKANI ZASONGA MBELE KUKAMILISHA MAKUBALIANO MAKUBWA YA UWEKEZAJI

Image
RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, katika Ikulu ya Chamwino, kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano na kuimarisha dhamira ya pamoja ya kujenga ushirikiano wa kisasa na wenye manufaa kwa pande zote mbili. Balozi Lentz—aliyefuatana na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa na Uchumi—amesisitiza dhamira ya Washington kuhuisha mahusiano na kuongeza kina la ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kiusalama kati ya mataifa haya mawili. “Marekani imejitolea kujenga ushirikiano usiotegemea misaada, bali unaojengwa juu ya ustawi wa pamoja,” alisema Balozi Lentz. Mazungumzo yamejikita katika hatua za majadiliano ya miradi mikubwa inayoongozwa na kampuni za Marekani. Pande zote mbili zimekubaliana kuwa majadiliano ya miradi miwili ya kimkakati—Mradi wa LNG na Mradi wa Tembo Nickel—yamefikia hatua za mwisho kabla ya kutiwa saini rasmi. Uwekezaji wa tatu, Mradi wa Mahenge Graphite, unaen...

JONATHAN BUDJU AFUNGA MWAKA NA ITURI

Image
Jonathan Budju afunga mwaka na 'Ituri Amani' Na Bright Davis Mwimbaji nyota wa Injili kutoka nchini Canada, Jonathan Budju, ameweka wazi kuachia wimbo mpya hivi karibuni maalumu kuhamasisha amani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Budju amejizolea umaarufu mkubwa kwenye muziki wa Injili pamoja na kujihusisha na masuala ya kijamii kupitia taasisi yake ya JB Foundation inayofanya kazi Afrika Mashariki. Akizingumza na gazeti hili, Jonathan amesema wimbo huo utatoka Disemba 19, akiwa ameshirikiana na waimbaji wa Ituri Gospel Artist na utaitwa Itune Amani. "Lengo ni kuendelea kuhamasisha amani Mashariki mwa DRC maeneo ya Ituri na Kivu, naamini wimbo utagusa wengi na kubadilisha maisha yao, nitatoa video na audio kwa pamoja katika platforms zangu zote za muziki," amesema Jonathan.

MSAMA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA HOTUBA YENYE KUIMARISHA UMOJA NA AMANI

Image
Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa hotuba yake iliyojaa hekima na weledi aliyoitoa mbele ya wazee wa Dar es Salaam. Msama amesema hotuba hiyo imeonyesha uwazi, ufasaha na dhamira ya dhati ya kulinda amani na utulivu wa Taifa. “Hakuna kiongozi anayetamani wananchi wake wapate shida au mashaka. Kila kiongozi mwenye busara hutaka kuona watu wake wakiishi kwa upendo, umoja na amani,” amesema Msama. Akitolea mfano kitabu cha Wafalme katika maandiko matakatifu, Msama alisema ni muhimu kwa wananchi kuheshimu maagizo na mamlaka zilizopo kwa manufaa ya Taifa. Amesisitiza pia umuhimu wa vijana kuondoa hofu na kuendelea kuheshimu mihimili ya nchi ikiwemo Rais, Bunge na Mahakama. Aidha, Msama aliwataka wazee kuzungumza na watoto na wajukuu wao ili kuhakikisha hawaingii katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani ya nchi. “Methali inasema: ‘Asiyefunzwa na wazazi hufunzwa na ulimwengu’. Nawaomba wana...

MSIMU WA AFCON 2025 DSTV KUONESHA MECHI ZOTE

Image
Msimu wa AFCON 2025 wazinduliwa; DStv kuonesha mechi zote 52 ikiwemo za Taifa Stars DAR ES SALAAM:MSIMU wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) umezinduliwa rasmi, ambapo DStv imethibitisha kuonyesha mubashara mechi zote 52, ikiwemo mechi za kundi la Taifa Stars, hatua ambayo imepokelewa kwa shamrashamra na mashabiki wa soka nchini. Maandalizi ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika yanaendelea kupamba moto kuelekea kuanza kwake tarehe 21 Desemba 2025 hadi 18 Januari 2026 nchini Morocco. Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni “Wanafamilia Tuna Kikao Chimbo ni SuperSport”, Mkuu wa Masoko wa DStv Tanzania, Ronald Shelukindo, amesema dhamira ya DStv ni kuhakikisha Watanzania wanafuatilia kwa ukaribu michuano hiyo na kufurahia utamaduni wa soka la Afrika. Ameeleza kuwa "Mechi zitatolewa kwa lugha mbalimbali ikiwemo Kiswahili, Kiingereza, Kireno, Kifaransa na lugha za Kiafrika, ili kuhakikisha mashabiki wanapata burudani kwa uelewa mpana zaidi. Katika hatua y...

WAHITIMU UDSM WAHIMIZWA KULINDA AMANI

Image
Wahitimu UDSM Wahimizwa Kulinda Amani na Kutumia Elimu Kuendeleza Taifa Katika duru ya nne ya mahafali ya 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), jumla ya wahitimu 2,046 kutoka ngazi mbalimbali za masomo walitunukiwa vyeti na shahada, zikiwemo Shahada ya Uzamivu, Shahada ya Umahiri, Stashahada ya Uzamili, Shahada ya Awali, Stashahada na Astashahada. Sherehe hizo zilizofanyika leo Desemba 1, 2025 jijini Dar es Salaam, zilitawaliwa na ujumbe wa kuhimiza vijana kulinda amani, kuendeleza mshikamano na kuutumikia vyema ujuzi walioupata kwa manufaa ya Taifa. Akizungumza katika mahafali hayo, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa William Anangisye, alisema uhai, usalama na maendeleo ya Taifa lolote duniani yanategemea nguvu ya vijana, hivyo ni wajibu wao kutumia ujana kwa manufaa ya jamii. “Hakuna asiyejua mchango wa vijana katika Taifa. Tumieni ujana wenu kwa faida na msichoke kulinda amani popote mlipo,” amesema Prof. Anangisye. Amesisitiza kuwa elimu waliyoipata inapaswa kuone...

MSAMA: TUWAPUUZE WANAOLIPWA KUVURUGA AMANI YETU*

Image
Mfanyabiashara malufu nchi Tanzania Ndugu Alex Msama amewataka Watanzania kuwapuuza watu ambao wanalipwa ili kuvuruga amani ya nchi yetu ya Tanzania na mara nyingi sio Watanzania na baadhi yao ni Watanzania wanaoishi nje ya nchi kama vile Kenya na mataifa mengine ya nje. "Watanzania wenzangu, nawasihi kwa moyo mmoja tuwapuuze watu wanaotaka kuvuruga amani yetu, maana watu hawo wanalipwa Mamilioni ili kuvuruga amani yetu tuliyo nayo pia watu hawo hawaishi hata hapa nchini bali wanaishi nje ya nchi, wengi sio Watanzania na wanalipwa na baadhi ya Watanzania na watu wengine wa nje ya nchi ili wavuruge amani yetu iliyoasisiwa na wazee wetu , watu hawo furaha yawo nikuona amani yetu inavurugika ili watuibie Rasilimali zetu, pia furaha yao ni kuona tunagombana, tunauana na kuchukiana, tuwapuuze"

MSAMA ATOA WITO KWA WAZAZI, VIONGOZI WA DINI KUWALINDA VIJANA DHIDI YA VURUGU

Image
ALEX MSAMA WITO KWA WAZAZI, VIONGOZI WA DINI KUWALINDA VIJANA DHIDI YA VURUGU MKURUGENZI wa Msama Promotion, Alex Msama, ameetoa wito kwa wazazi nchini kukaa karibu na watoto wao na kuwashauri kuepuka ushawishi wa kujiingiza kwenye vitendo vya vurugu na misukumo isiyo na tija. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Msama alisema wazazi wana jukumu kubwa la kuhakikisha vijana wanalelewa katika misingi ya maadili na uzalendo, kwa kuwa wao ndio wamewazaa na kuwalea. “Mimi kama mzazi niseme kuwa watoto ni wetu, tumewazaa na kuwalea. Tuna uwezo wa kukaa nao, kuzungumza nao na kuwaonya. Tusikubali waingie kwenye mkumbo wa kufanya vurugu,” amesema Msama. Amesisitiza kuwa hakuna mtu mwenye mapenzi ya dhati kwa Tanzania zaidi ya Watanzania wenyewe, hivyo ni muhimu kuepuka kufuata mkumbo usio na manufaa kwa taifa. “Amani tuliyonayo ni ya muhimu sana. Tumeachiwa na waasisi wetu, wazazi na mababu zetu. Tunapaswa kuilinda kwa nguvu zetu zote,” ameongeza. Msama ...

OSMAN AAHIDI KUMCHAPA MAZOMBE

Image
Osama aahidi kum hapa Mazome mapema Na Brigitte Davis DAR ES SALAAM: BONDIA kutoka Mtwara, Osama Alabi, ambaye ameweka kambi yake ya maandalizi Mazense ametangaza kumkalisha mpinzani wake Ally Mazome wa Morogoro kwa TKO katika pambano la Boxing on Boxing Day litakalofanyika Desemba 26, 2025 katika Ukumbi wa Warehouse, Masaki. Akizungumza m Dar es Salaam , Alabi anayefahamika pia kama Osama Korosho amesema amejipanga vizuri kuhakikisha anapata ushindi katika pambano hilo akisisitiza kuwa mashabiki wa Mtwara na Watanzania kwa ujumla wawe sehemu ya “historia mpya” ambayo anatarajia kuiandika ulingoni. “Nimejiandaa vya kutosha, naimani hii ndiyo siku yangu. Naomba mashabiki wangu wote wa Mtwara na Watanzania waje kushuhudia ushindi wa kihistoria,”alisema. Kwa upande wa mashabiki wake, wameeleza kujiamini kuwa Osama ataibuka na ushindi mnono wakifananisha uwezo wake na “paka aliyekula mboga ya familia.” “Tumejiandaa, Osama anashinda bila shaka,” — Eliud Mwakapala (Shabiki) “Siku ...

DAR CITY WARUDI WAKIWA WAMESHINDA NAFASI YA 3

Image
Nahodha wa Dar City: “Mchezo Ulikuwa Mgumu, Lakini Tumepambana Mpaka Mwisho” NAHODHA wa Timu ya Basketball ya Dar City, HasheemThabit, amesema mashindano waliyoshiriki nchini Kenya yalikuwa na ushindani mkubwa, lakini wanashukuru kwa nafasi waliyoipata na matokeo waliyofikia. Akizungumza mara baada ya kurejea nchini, Thabiti amesema mchezo wa basketball una siku zake, na si kila mara matokeo huwa upande mmoja. “Basketball ni mchezo wa tofauti; si kila siku mchezo utakuwa wako. Kuna siku utaongoza, na kuna siku utapata changamoto. Wachezaji gani tunawahitaji, tunaweza kuendelea nao, na wapi wanauwezo mdogo hayo yote tunapaswa kuyapima,” amesema Thabiti. Nahodha huyo ameendelea kusisitiza kuwa ameshinda michezo mingi ya basketball na anaifahamu vema namna mchezo unavyobadilika kulingana na mazingira na ubora wa timu pinzani. Klabu ya Dar City ilishukuru Mungu kwa mafanikio waliyoyapata katika mashindano hayo, ikiwemo kushika nafasi ya tatu, ikiwa ni ishara ya uwakilishi m...

DAR CITY WAMEFUZU HATUA BAADA YA USHINDI VIKAPU 92 KWA 77

Image
Timu ya mpira wa Kikapu ya Dar City leo imeandika historia mpya baada ya kufanikiwa kuwa timu ya kwanza ya Tanzania kufuzu kucheza fainali za BAL 2026 (Basketball African League). Dar City wamefuzu hatua hiyo baada ya ushindi wa vikapu 92-77 dhidi ya Club Ferroviario ya Msumbiji, Dar City wamemaliza nafasi ya tatu katika hatua ya Elite 16.

DAR CITY YAFIKA NUSU FAINALI AFRIKA

Image
KLABU ya Dar City imeweka historia mpya baada ya kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya kufuzu Fainali za Ligi ya Afrika, kufuatia rekodi ya ushindi katika michezo yake yote mitatu ya Kundi B. Katika mchezo wa kwanza, Dar City ilianza kwa kishindo baada ya kuichapa Matera Magic kwa pointi 85–78, kabla ya kuendeleza ubabe kwa kuilaza Brave Hearts kwa 93–75. Timu hiyo kutoka Tanzania ilikamilisha hatua ya makundi kwa ushindi mwingine muhimu dhidi ya Ferroviario kwa 87–78, na kujihakikishia nafasi kileleni mwa kundi. Kutokana na matokeo hayo, Dar City sasa inasubiri kukutana na timu itakayomaliza katika nafasi ya pili kwenye Kundi B, pambano litakalokuwa na ushindani mkubwa kutokana na ubora uliooneshwa na kikosi hicho tangu mwanzo wa mashindano. Dar City iwapo itafanya vizuri katika hatua hiyo ya nusu fainali basi itakuwa ni miongoni mwa timu tatu zitakazowakilisha kwenye fainali za ligi ya kikapu Afrika zitakazofanyika Kigali, nchini Rwanda mwakani.

STEVE NYERERE NA ASASI WAKABIDHI MILION TANO MSIBA WA MC PILIPILI.

Image
MWENYEKITI wa Taasisi ya Mama Ongea Na Mwanao Steve Mengele iSteve Nyererei amesema Pilipili ameondoka kipindi ambacho taifa linamuhitaji. Akizungumza wakati wa Salamu za Pole Kwa Familia, Ndugu, Jamaa na Marafiki wa Marehemu MC PiliPili Nchi Nzima inamlilia. Aidha kama Mama Ongea na Mwanae wametoa kiasi cha Sh Milioni tano kitaka endakusaidia elimu kwa watoto wa marehemu Mc Pilipili. Steve Nyerere Ameeleza Kuumizwa Sana na Kifo Cha Mc PiliPili Ikiwa Kama Nchi Imempoteza Mtu mahiri Sana. "PiliPili ameondoka muda ambao kama nchi ilikuwa inamuhitaji kuongeza nguvu kazi"amesema Marehemu MC PiliPili Amezikwa Leo Jioni Huko Jijini Dodoma,Tanzania.

NICE TO MEET YOU MSIMU WA PILI HUKU LIPA TUKUBUSTI

Image
“‘Nice to Meet You’ Yazindua msimu wa pili, wasanii watakiwa kuongeza viwango kuboresha filamu za Tanzania” TAMTHILIA maarufu Nice to Meet You imemtambulisha rasmi msanii mpya, Tasu, katika uzinduzi wa msimu wake wa pili, huku wadau wa filamu nchini wakihimiza utengenezaji wa kazi zenye ubora na viwango vya kimataifa ili kukuza hadhi ya soko la filamu Tanzania na kuinua vipaji vipya. Akizungumza katika uzinduzi huo, Munirah Pendeza, 'Tusa' ndani ya tamthilia hiyo, amesema sekta ya filamu kwa sasa imekuwa na hamasa, morali na motisha kubwa miongoni mwa watayarishaji, hivyo wasanii wanapaswa kufanya kazi kwa ubora zaidi ili kuendana na kasi hiyo. Tusa amewahimiza mashabiki kutumia ofa maalumu ya msimu wa sikukuu kwa kulipia ving’amuzi vya StarTimes, ili kufurahia maudhui mbalimbali ikiwemo tamthilia ya Nice to Meet You, katuni za watoto kama Bonnie Bears (maarufu kama Kipara Mbabe), Super Wings, pamoja na maudhui ya michezo na tamthilia zilizotafsiriwa kwa Kiswahili. Kwa up...

JK AONGOZA MAHAFALI YA 55 (DURU LA PILI) YA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM UKUMBI WA MLIMANI CITY JIJINI DAR

Image
UDSM yamtunuku Dkt. Maria Kamm Shahada ya Heshima kutokana na mchango wake katika elimu nchini DAR ES SALAAM MKUU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ametunuku Shahada za Awali, Stashahada na Astashahada kwa wahitimu katika Mahafali ya 55 (Duru la Pili) ya chuo hicho kikongwe kuliko vyote nchini. Jumla ya wahitimu 2,742 walihudhurishwa kwenye mahafali hayo yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. katika hatua nyingine Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimemtunuku Digrii ya Heshima ya Udaktari wa Fasihi Mwasisi na Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Clementina, Dkt. Maria Josephine Kamm, kutokana na mchango wake mkubwa na wa muda mrefu katika kuendeleza elimu nchini. Tuzo hiyo imetolewa leo, Novemba 18, 2025, wakati wa mahafali ya 55 ya UDSM yaliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City, yakihudhuriwa na maelfu ya wahitimu, wazazi na wageni waalikwa. Akizungumza baada ya kutunukiwa, Dkt. ...

STEVE NYERERE: DARAJA LA JAMII NA MWANAHARAKATI WA MAENDELEO

Image
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steven Waiton Mengele, maarufu kama Steve Nyerere, ni miongoni mwa wadau muhimu wa maendeleo nchini kupitia mchango wake mkubwa katika sanaa za maigizo na uchekeshaji kwa miaka mingi. Kwa muda mrefu, Steve ameendelea kuwa nguzo kwa makundi mbalimbali yenye uhitaji, wasanii na wadau wa sanaa kwa ujumla, akihakikisha anakuwa daraja la kusaidia na kuunganisha watu wanaohitaji msaada kwa namna moja au nyingine. Kupitia jitihada zake binafsi pamoja na ushirikiano kutoka kwa wadau wa ndani na nje ya nchi, amefanikiwa kupunguza au kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watu aliofikiwa. Rekodi zinaonesha kuwa Steve amekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha upatikanaji wa misaada ya hali na mali kwa watu wengi, hususan pale ambapo jambo liko ndani ya uwezo wake kulishughulikia. Nia yake thabiti ya kuleta mabadiliko chanya imeendelea kumjengea uaminifu mkubwa kutoka kwa taasisi, viongozi, wadau na jamii, kiasi cha kutazamwa kama da...

AFRICA KUKUTANA ARUSHA MKUTANO WA TEKNOLOJIA YA AKILI MNEMBA (APAIC 2025) NOVEMBA 24 HADI 27

Image
Washiriki zaidi ya 1,200 kutoka nchi zaidi ya 40 wanatarajiwa kushiriki Mkutano wa Kilele wa Akili Unde Afrika (APAIC 2025) utakaofanyika jijini Arusha kuanzia Novemba 24 hadi 27, 2025, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC). Mkutano huo unatarajiwa kuwa jukwaa muhimu la kimataifa litakalojadili matumizi ya teknolojia ya Akili Mnemba (Unde) katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, kilimo, biashara na utawala bora. Akizungumza kuhusu maandalizi ya mkutano huo, Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa APAIC 2025, Abdulwahid Ali Khamis, alisema tukio hilo litaweka historia mpya katika safari ya mageuzi ya kidijitali barani Afrika, likilenga kuunganisha serikali, sekta binafsi, wawekezaji, taasisi za elimu na wabunifu wa teknolojia. “Afrika ipo katika kipindi muhimu cha kuamua njia ya mageuzi yake ya kijamii na kiuchumi kupitia akili unde. Huu ni wakati wa kuweka misingi ya matumizi jumuishi, bunifu na yenye maadili ya teknolojia hiyo,” amesema Khamis. Amee...

AFRICA KUKUTANA ARUSHA MKUTANO WA TEKNOLOJIA YA AKILI MNEMBA (APAIC 2025) NOVEMBA 24 HADI 27

Image
Washiriki 1,200 kuhudhuria mkutano wa teknolojia ya Akili Unde Afrika (APAIC 2025) Arusha Washiriki zaidi ya 1,200 kutoka nchi zaidi ya 40 wanatarajiwa kushiriki Mkutano wa Kilele wa Akili Unde Afrika (APAIC 2025) utakaofanyika jijini Arusha kuanzia Novemba 24 hadi 27, 2025, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC). Mkutano huo unatarajiwa kuwa jukwaa muhimu la kimataifa litakalojadili matumizi ya teknolojia ya Akili Mnemba (Unde) katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, kilimo, biashara na utawala bora. Akizungumza kuhusu maandalizi ya mkutano huo, Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa APAIC 2025, Abdulwahid Ali Khamis, alisema tukio hilo litaweka historia mpya katika safari ya mageuzi ya kidijitali barani Afrika, likilenga kuunganisha serikali, sekta binafsi, wawekezaji, taasisi za elimu na wabunifu wa teknolojia. “Afrika ipo katika kipindi muhimu cha kuamua njia ya mageuzi yake ya kijamii na kiuchumi kupitia akili unde. Huu ni wakati wa kuweka misingi...