Posts

Showing posts from September, 2024

MSHINDI WA MPIRA MREFU KUONDOKA NA GARI

Image
Mashindano ya gofu ya Kombe la Mkuu wa Majeshi ‘NMB CDF Trophy’ yanatarajiwa kufanyika Oktoba 4-6,2024, huku mchezaji atakayefanikiwa kupiga ‘hole in one’ atapewa zawadi ya gari aina ya Toyota Harrier yenye thamani ya sh milioni 70 na kwenda kupumzika hoteli ya Serena . Gari hiyo imekabidhiwa leo Septemba 27,2024 na Meneja Mkuu wa Toyota kwa kwa Mwenyekiti wa Klabu ya Gofu Lugalo, jijini Dar es Salaam, Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo. Akizungumzia mashindano hayo yatakayofanyika katika viwanja vya klabu Lugalo, Brigedia Jenerali Mstaafu Luwongo amesema mchezaji atayepiga ‘hole in one’ atakabidhiwa gari yake muda huo huo na italipiwa kila kitu. Ameeleza lengo mashindano kuwa ni kumuenzi mlezi wa klabu ambaye ni Mkuu wa Majeshi ambapo kwa sasa ni Jenerali Jacob Mkunda na siku ya kufunga ndiye atakuwa mgeni rasmi. Amesema kuwa pamoja kumuenzi Mkuu wa Majeshi lakini pia ni muendelezo wa sherehe za kuzaliwa kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambayo kila mwaka huadh...

FANYA MUAMALA UPATE ELFU 20000

Image
Watumiaji wa mtandao wa Airtel nchini wameshauriwa kutumia huduma ya Airtel money ili kuweza kupata nafasi ya kujipatia shilingi 20,000/=, kwa kufungua huduma ya Artel money kwa namba au Airel Money App ndani ya miezi mitatu. Mkurugenzi wa mawasiliano Jackson Mbando anasema kampeni hiyo itadumu kwa muda wa miezi mitatu na watumiaji wote wa mtandao huo watapata nafasi ya kupata kiasi hicho mara tu baada ya kufungua Airtel Money. Wadau mbalimbali wakiwemo Waandishi wa Habari walijitokeza mapema leo Septemba 26, 2024, kushuhudia uzinduzi wa kampeni mpya ya AirtelMoney Jiboost yenye lengo la kuku-boost pindi unapofanya miamala na AirtelMoney! Mr Money na Simba wanakuambia sasa utapata elfu 20,000 kadiri unavyofanya miamala, kutuma pesa Airtel kwenda Airtel au kununua muda wa maongezi kupitia AirtelMoney ufaidi supa bonasi!