AZAM TV YAZINDUA KAMPENI YA "USALAMA DAIMA" KUOKOA MAISHA YA MADEREVA BODABODA
Azam Media Yazindua Kampeni ya “Usalama Daima” Kuokoa Maisha ya Madereva Bodaboda Kampuni ya Azam Media Limited imezindua rasmi kampeni ya usalama barabarani yenye kauli mbiu “Usalama Daima, Azam TV Milele”, ikiwa na lengo la kutoa elimu na ujuzi kwa watumiaji wa vyombo vya moto, hususan madereva wa bodaboda, ili kupunguza ajali zinazoweza kuepukika. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika Kimara, Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, Afisa Uendeshaji Mkuu wa Azam Media Limited, Yahya Mohamed, alisema kuwa kampeni hiyo inalenga kuwajengea uwezo madereva kwa kuwapatia mafunzo maalum pamoja na nyenzo muhimu za usalama barabarani. Ameeleza kuwa utekelezaji wa kampeni hiyo utaendelea katika maeneo mbalimbali nchini hadi kufikia mwezi Septemba mwaka huu, huku madereva bodaboda wakihusishwa moja kwa moja ili kuhakikisha wanapata elimu ya matumizi salama ya barabara pamoja na umuhimu wa vifaa kinga. Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Divisheni ya Maso...