AJIRA ZAIDI YA 2000 ZATENGENEZWA MAONESHO YA AJIRA YA CHINA NCHINI TANZANIA 2025
Wizara ya Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wafanyabiashara wa China wanaofanya shughuli zao nchini, imeingia makubaliano ya kutoa ajira kwa zaidi ya vijana 2,000 wa Kitanzania, ikiwa ni juhudi za kutatua changamoto ya ajira nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu),Ridhiwani Kikwete, amesema kuwa ushirikiano huo unalenga kuwawezesha vijana kufahamu aina ya ajira zilizopo kupitia kampuni mbalimbali za Kichina zinazofanya kazi nchini Tanzania. "Kwanza kabisa, kijana anapaswa kufahamu aina ya ajira zilizopo na kuweza kuchangamkia nafasi hizo kupitia makampuni yaliyo tayari kuajiri. Lengo kuu ni kupunguza changamoto ya ajira na kuwawezesha vijana wetu," amesema Ridhiwani Kikwete. Aliongeza kuwa Wizara inasisitiza ushiriki wa vijana kwa wingi ili kunufaika na nafasi hizo, ambapo baadhi ya mchakato wa mahojiano (in...