WASHIRIKI 20 BSS WATINGA KAMBINI
Washiriki 20 watinga kambini Bongo Star Search DAR ES SALAAM: WASHIRIKI 20 kutoka Kenya Uganda Congo na Tanzania waliochaguliwa kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania pamoja na nchi kadhaa za Afrika Mashariki na Kati wamewasili rasmi kambini katika ufukwe wa Ndege Beach jijini Dar es Salaam kuanza safari yao ya kutwaa ushindi vipaji la Bongo Star Search (BSS). Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Azam Media jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Benchmark Production na muandaaji wa shindano hilo, Rita Paulsen, amesema msimu wa mwaka huu umebeba ushindani mkubwa zaidi kutokana na kiwango cha juu cha vipaji vilivyojitokeza wakati wa usaili. Rita amesema kundi hilo linajumuisha Watanzania 10, Wakenya watatu, Waganda wawili, Wakongo watatu, pamoja na kundi moja la wachezaji wa dansi na mchekeshaji mmoja kutoka Mbeya. “Washiriki wa mwaka huu wana viwango vya juu sana. Kuna tofauti kubwa ukilinganisha na misimu iliyopita, jambo linaloonesha ukuaji wa sekta ya buruda...