WAAJIRI WAIMIZWA KUONGEZA NA KUZINGATIA UTU MAHALA PA KAZI
WAAJIRI WAIMIZWA KUONGEZA NA KUZINGATIA UTU MAHALA PA KAZI Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewahimiza waajiri nchini kuongeza umakini na kuzingatia misingi ya utu mahali pa kazi ili iwe motisha na chachu kwa watumishi kuongeza ubunifu na ufanisi kazini. Dkt. Biteko amesema hayo wakati akimwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Phillip Mpango katika usiku wa Tuzo kwa mwajiri Bora wa mwaka 2024 ambapo Kampuni ya bia nchini (TBL) imeibuka mshindi wa jumla ikifuatiwa Kampuni ya Barick Gold huku Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA ikishika nafasi ya tatu. Amewapongeza waandaaji wa tuzo hizo na kuwataka kupanua wigo wa makundi ya ushiriki huku akisisitiza umuhimu wa utoaji wa motisha mahala pa kazi ili watumishi waongeze ari ya kufanya kazi kwa viwango na ubora wajuu. “ mwajiri anachokihitaji kwa mwajiriwa ni muda na ujuzi wake basi. Hivyo, waajiri ongezeni umakini na utu mahali pa kazi na mkifanya hivyo...