Posts

Showing posts from 2024

NABII MALISA AMSHUKURU DKT SAMIA KWA KURUHUSU HUDUMA ZA KIROHO

Image
  CHUNGAJI wa Kanisa la Madhabau ya Hatma, Nabii Clear Malisa, amemshukuru Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan kwa serikali yake kwa kutoa uhuru wa kuabudu bila kuchagua. Malisa ameyasema hayo mapema leo Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuzungumzia mkesha mkubwa unaotarajia kufanyika leo kanisani kwake  Ubungo Kibangu. "Rais Samia amekuwa na ushirikiano mkubwa kwetu viongozi wa dini, tunamshukuru kutobagua dhehebu lolote"amesema Malisa. Hata hivyo, Malisa ameutabiri mwaka 2025 utakuwa mwaka wa neema zaidi kwa Taifa la Tanzania katika nyanja ya uchumi  ikiwemo kupanda kwa shilingi ya Tanzania dhidi ya Dola za Kimarekani. Pia ameongeza kwa kutoa utabiri anaofanya, kiongozi huyo kwa kiroho amesema ni Utashi ambao Mungu amempa na kuhaidi kutoa utabiri juu ya mambo mbalimbali ikiwemo uchaguzi mkuu wa hapo mwakani kupitia kwenye mkesha utakaofanyika kanisani leo. Aidha Nabii  Malisa amewataka watanzania kipindi hiki cha...

TGNP WASHEHRREKEA MIAK 30 YA BEIJINGNA DIRA 2050

Image
 Na Brighitte Davis  MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP) umesherehekea miaka 30 ya Beijing katika kongamano la wanawake na uongozi Dar es Salaam leo huku ukihimiza umuhimu wa wanawake kuendelea kujitokeza kwa wingi  katika uchaguzi mkuu ujao kugombea nafasi mbalimbali za uongozi. Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Lilian Liundi amesema wanayo furaha kuona uchaguzi wa serikali za mitaa namna wanawake wengi wameitikia na kushika nafasi za wenyeviti akisema anaamini data zitaendelea kuongezeka. Amesema takwimu zinaonesha asilimia 6.5 tu ya wanawake waliochaguliwa kwenye uchaguzi wa 2019 ni madiwani, na kwamba asilimia 2.1 ya wanawake waliochaguliwa Tanzania nzima walishika nafasi ya wenyeviti wa vijiji, 6.7 wenyeviti wa vitongoji na 12.6 wenyeviti wa mtaa, takwimu hizo zikionesha hawajafikia asilimia wanazotazamia. “Tunayo imani kwamba kuna uchaguzi wa mwaka ujao data zitakuwa tofauti lakini hapa tunayo mifano ya wanawake waliopasua miamba kwenye uchaguzi...

EWURA YAPIGA MARUFUKU KUKATWA MAJI WEKENDI

Image
  Na Brigitte Davis MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imesema ni  marufuku kwa mamlaka za maji nchini kukata maji mwishoni mwa wiki kwasababu kufanya hivyo ni kama unyanyasaji. Hayo yamesemwa Dar es Salaam leo  na Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Umma  wa EWURA, Titus Kaguo kwenye semina kwa Chama cha Wafanyakazi wa Vyombo vya habari nchini (JOWUTA). Amesema kitendo cha mtu kukatiwa maji kuanzia Ijumaa saa 12  jioni au Jumamosi na Jumapili hairuhusiwi kiutaratibu na kiudhibiti.  "Mtu anayefanya hivyo asifanye tena kwasababu anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria ili kuwajibika kwa kile anachokifanya,"amesema. Amesema Watanzania wajenge utamaduni wa kusoma mikataba ya huduma kwa wateja kwani inawapa wajibu wa wao wafanye nini na mamlaka zifanye nini. Kaguo amesema mamlaka zimekuwa hazihamasishi mikataba hiyo ili Watanzania wasiibuke na kuanza kudai haki zao. Pia, amesema  kuwa wakati wa usomaji wa mita za maji, ofisa wa mamlaka y...

URBAN BY CITY YASHINDA TUZO YA HOTEL BORA

Image
  Urban by CityBlue, Dar es Salaam Yashinda Tuzo ya Consumer Choice kwa Hoteli Bora ya Huduma Bora na Mwangaza nchini Tanzania (4-Star) Urban by CityBlue, Dar es Salaam, sehemu ya portifolio maarufu ya CityBlue Hotels, imetunukiwa Tuzo ya Consumer Choice kwa Hoteli Bora ya Huduma Bora na Mwangaza nchini Tanzania (4-Star). Tuzo hii ya heshima inatambua muundo wa kipekee wa hoteli, uzoefu wa kipekee wa wageni, na dhamira ya kutoa huduma za kiwango cha kimataifa. Iko katikati ya jiji lenye vionjo vya maisha ya Dar es Salaam, Urban by CityBlue imekuwa ikisherehekewa kwa uzuri wake wa kisasa, vifaa vya kisasa, na ukarimu wa Kitanzania. Kutambuliwa kwa hoteli hii kunasisitiza kujitolea kwake katika kuweka viwango vipya katika tasnia ya huduma za kifahari katika kanda hii. Khalil Hamadi, mkurugenzi wa kampuni inayosimamia Urban by CityBlue, Dar es Salaam alisema: “Tunajivunia kuona mafanikio haya, ambayo yanatufanya kuendelea kuhamasika na kupiga hatua kubwa zaidi katika ubora wa huduma n...

KAMPUNI YA JAN INTERNATIONAL IMETUNZA WATEJA WAKE

Image
Kampuni ya kuuza magari ya Jan international Ltd imewatunza wateja wake  wanne gari, pikipiki, jokofu na simu ikiwa ni sehemu  ya kurudisha kwa jamii na kuwashukuru kwa kuwaunga mkono. Washindi hao wametokana na droo waliyoichezesha juzi baada ya kampeni ya kuendesha zoezi hilo iliyofanyika kwa zaidi ya mwezi mmoja kwa kukusanya karasi walizopewa wajaze watu wote waliokwenda kununua magari kwenye kampuni hiyo. Washindi hao ni Edwin Godwin alishinda gari aina ya Harrier anaconda, Harun Rajabu alishinda pikipiki, Agnes Nganile alishinda jokofu na tv inchi 52 na Issa Tambuu alishinda simu aina ya Iphone 16 pro max. Mshindi wa gari Godwin alisema ametoka kununua gari mwezi uliopita na wakati anapewa karatasi ajaze hakuamini alikuwa anaona kama anapoteza muda wake akiamini huwa wanachaguliwa na kueleza furaha yake baada ya kuona ni kweli. "Mwanzoni sikuamini kumbe ni kweli, nashukuru sana Jan kwa kututhamini wateja wao msimu huu wa sikukuu mmetutia moyo na kutuhamasisha kuendelea k...

DULLA MBABE KUSAFISHA NGUMI MAUGO

Image
 Na Brighitte Davis BONDIA wa ngumi za kulipwa, Abdallah Pazi 'Dullah Mbabe' amesema anaenda kumstafisha  ngumi mpinzani wake, Mada Maugo katika pambano la 'Taji la Mama Samia' litakalofanyika Desemba 26, mwaka huu. Dullah Mbabe atapanda ulingoni kuzichapa pambano kuu  dhidi ya Maugo la raundi nane, uzito wa juu ( kilo 76) litakalofanyika Muleba Mkoani Kagera. Akizungumza Dar es Salaam leo katika uzinduzi wa pambano hilo, Dullah Mbabe amesema baada ya kukaa kimya muda mrefu bila kupanda ulingoni awamu hii amejipanga kuja kuleta mapinduzi  katika ngumi kwa kumchakaza mkongwe huo mwenzake. "Nimejipanga  salama kiafya naendelea vizuri, naenda katika vita dhidi ya Mada Maugo, baada ya kupoteza mapambano machache ikiwemo la Erick Katompa naenda kuonyesha kazi mkoani Kagera,"amesema. Amewatoa hofu wakazi wa Muleba na kuwataka wakae mkao wa kula wategemee mambo mazuri kutoka kwake kwani siku hiyo atamuonyesha kazi kwa sababu mara ya kwanza alimtengua  kiuno awamu ...

WAAJIRI WAIMIZWA KUONGEZA NA KUZINGATIA UTU MAHALA PA KAZI

Image
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewahimiza waajiri nchini kuongeza umakini na kuzingatia misingi ya utu mahali pa kazi ili iwe motisha na chachu kwa watumishi kuongeza ubunifu na ufanisi kazini. Dkt. Biteko amesema hayo wakati akimwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Phillip Mpango katika usiku wa Tuzo kwa mwajiri Bora wa mwaka 2024 ambapo Kampuni ya bia nchini (TBL) imeibuka mshindi wa jumla ikifuatiwa Kampuni ya Barick Gold huku Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA ikishika nafasi ya tatu.  Amewapongeza waandaaji wa tuzo hizo na kuwataka kupanua wigo wa makundi ya ushiriki huku akisisitiza umuhimu wa utoaji wa motisha mahala pa kazi ili watumishi waongeze ari ya kufanya kazi kwa viwango na ubora wajuu.  “ mwajiri anachokihitaji kwa mwajiriwa ni muda na ujuzi wake basi. Hivyo, waajiri ongezeni umakini na utu mahali pa kazi na mkifanya hivyo, waajiriwa ambao wanatumia muda mwingi kazini, wataongeza ubunifu na ufanisi ...

MFALME MZEE YUSUPH KUPEWA MAUWA YAKE DISEMBA 8

Image
  MSANII  wa muziki wa taarabu nchini Mzee Yusuph ‘Mfalme wa Taarabu’ anatarajia kupewa mauwa yake kwa kuupigania muziki huo katika tamasha  la muziki huo linalotarajia kufanyika Disemba 8, 2024 jijini Dar es Salaam. Akizungumza na habarileo Mzee Yusuph alisema kuwa watu wengi wanapenda kuwapa watu mauwa yao wakiwa wametangulia mbele za haki kwake ni tofauti. “Napewa mauwa yangu na ninayapokea kwa sababu najuwa kuwa nastaili maua haya, nimefanya muziki wa taabu kwa muda Mwingi lakini hakuna mwanaume yupo muda mrefu kwenye huu muziki zaidi yangu. "Mashabiki zangu na watu mbalimbali wanaopenda kazi zangu niwaombe na niwakaribishe katika tamasha maalumu la kunipa mauwa yangu kwa Mchango wangu kwenye tasnia ya muziki wa taarabu. “Kuna muda muziki wa taarabu ulikuwa kama umelala hakuna anayeweza kuuamsha kama Mzee Yusuph niwaambie tu watu wajitokeze kwa wingi Disemba 8 waone muziki unavyozaliwa upya huku nikipokea mauwa yangu.”alisema Mfalme Mzee Yusuph Aidha ameongeza kuwa at...

WAAJIRI WAIMIZWA KUONGEZA NA KUZINGATIA UTU MAHALA PA KAZI

Image
  WAAJIRI WAIMIZWA  KUONGEZA  NA KUZINGATIA UTU MAHALA PA KAZI Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewahimiza waajiri nchini kuongeza umakini na kuzingatia misingi ya utu mahali pa kazi ili iwe motisha na chachu kwa watumishi kuongeza ubunifu na ufanisi kazini. Dkt. Biteko amesema hayo wakati akimwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Phillip Mpango katika usiku wa Tuzo kwa mwajiri Bora wa mwaka 2024 ambapo Kampuni ya bia nchini (TBL) imeibuka mshindi wa jumla ikifuatiwa Kampuni ya Barick Gold huku Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA ikishika nafasi ya tatu.  Amewapongeza waandaaji wa tuzo hizo na kuwataka kupanua wigo wa makundi ya ushiriki huku akisisitiza umuhimu wa utoaji wa motisha mahala pa kazi ili watumishi waongeze ari ya kufanya kazi kwa viwango na ubora wajuu.  “ mwajiri anachokihitaji kwa mwajiriwa ni muda na ujuzi wake basi. Hivyo, waajiri ongezeni umakini na utu mahali pa kazi na mkifanya hivyo...

JUMUIYA ZA USAFIRISHAJI MAJINI WATAKIWA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA SEKTA YA USAFIRISHAJI

Image
  Jumuiya ya Mamlaka za Usimamizi wa Usafiri majini Barani Afrika zimetakiwa kushirikiana na kuungana ili kuimarisha usalama wa sekta ya usafirishaji majini na hivyo kuchochea maendeleo ya Uchumi katika nchi husika. Wito huo umetolewa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko Leo Disemba 29,2024 wakati akifungua Kongamano na Mkutano Mkuu wa mwaka wa Jukumuiya ya Mamlaka za Usimamizi na Usafirishaji Majini Barani Afrika unaofanyika kwa siku tatu, Jijini Dar es Salaam. Dkt. Biteko amewashauri washiriki kutumia mkutano huo kama fursa ya kubuni na kupanga mikakati mipya ya kuelekea katika mafanikio kupitia sekta hiyo ambapo amesisitiza kuwa ushirikiano miongoni mwa washiriki na kujadiliano juu ya kuwezesha masuala mbalimbali na sekta ya usafirishaji litakuwa suluhisho la changamoto mbalimbali zilizopo. “Kila mmoja wetu atumie fursa ya mkutano huu kujiwekea malengo yatakayo tuwezesha kufikia azima ya kuboresha usalama na kuimarisha sekta ya usafirishaji wa majini”...

MALKIA MWENYE CHOMBO YAZINDULIAWA RASMI MO FINANCE

Image
Wanawake mbalimbali watakiwa kujitokeza kuchukua mikopo ya bajaji itakayowasaidia kujikimu kimaisha ili wasiwe magoli kipaji kwenye familia zaoa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Melt  Group na Mo Finance Fatema Dewji amesema wamezindua rasmi Kampeni ya Malkia mwenye Chombo, mradi wa kipekee unaolenga kuwawezesha wanawake kwa kuwapatia Bajaj mpya kwa mkopo wa masharti nafuu.  "Mpango huu unaendeleza dhamira ya Melt ya kushiriki katika maendeleo ya jamii na kubadilisha maisha ya wanawake wengi kujikimu kimaisha na kuwa na maendeleo yao binafsi. “Malkia mwenye Chombo ni mwendelezo wa desturi ya METL ya kuinua jamii. Tuna furaha kuona familia nyingi sana zimewezeshwa kupitia miradi yetu, na kampeni hii ni hatua nyingine muhimu ya kuinua kundi kubwa zaidi.” "Anapochukua mkopo tuna hakikosha tunamlipia mafunzo ya udereva katika Chuo cha NIT na kumpatia mafunzo ya biashara kwa kumkutanisha na wafanya biashara mbalimbali watakaompa njia ya nini a...

RC CHALAMILA WANANCHI JITOKEZENI KWA WINGI KUPIGA KURA NOVEMBA 27, 2024

Image
Chalamila amesema Mkoa unajumla ya mitaa 564 ambayo itashiriki uchaguzi huo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa Hoteli ya Johari Rotana Wilaya ya Ilala amewataka wananchi hususani wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kupiga kura Novemba 27,2024 ili kupata kiongozi atakayewaletea maendeleo. Aidha RC chalamila amesema vituo vya uchaguzi vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni, Mkoa unajumla ya mitaa 564 ambayo itashiriki katika uchaguzi huo pia Mkoa umejipanga vizuri katika kuhakikisha unawafikia watu wengi zaidi kwa kuongeza vituo vya kupiga kura katika mitaa. Vilele amevitaka vyombo vya Habari kutoa taarifa sahihi za uchaguzi na kuhamasisha wananchi kupiga kura. Sanjari na hilo RC Chalamila amewataka wananchi pamoja na vyama vya siasa kushiriki uchaguzi huo kwa kuzingatia 4R za Rais Samia yenye maana ya Maridhiano, Ustamilivu, Mageuzi na Kujenga upya "Lazima tujenge siasa zenye ustamilivu, siasa ambayo tuna...

MSAMA KUMSOMESHA MTOTO WA MAREHEMU FREDY

Image
  MKURUGENZ I wa Msama Promotion Alex Msama amejitolea   mtoto wa  Marehemu Msanii wa Bongo Movie Fredy Gordon Kiluswa miaka mitatu. MKURUGENZI wa Msama Promotion Alex Msama amejitolea kumsomesha mtoto wa  Marehemu Msanii wa Bongo Movie Fredy Gordon Kiluswa miaka mitatu. Akizungumza Mshehereshaji katika msiba wa Fredy Mc Dkt Cheni amesema kuwa Msama ametoa ahadi hiyo baada ya Steve Mengere  'Steve Nyerere' kusema atamsomesha mtoto huyo kwa mwaka mmoja. "Msama amesema kuwa atampokea Steve Nyerere kwa kumsomesha mtoto huyo kwa mwaka mmoja ndipo Msama akasema atampokea Steve Nyerere kwa kumsomesha miaka mitatu jina la mtoto anayejulikana kwa jina la Kenzo ambaye kwa sasa yupo darasa la pili."amesema Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Msama Promotion Alex Msama amesema kuwa ameguswa na Msiba huo wa kijana mdogo hivyo ameamua kuchangia kumsomesha mtoto kama sehemu ya faraja kwa familia hiyo. "Ni kijana mdogo ameondoka mapema sana binafsi nimemfahamu kup...

TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA SABA WA TASAC USAFIRI MAJINI

Image
  Nagitte Davis  Dar es salaam. Tanzania  kupitia  shirika la uwakala  wa Meli Tanzania (TASAC) imeteuliwa  kuwa  nchi mwenyeji kwenye  wa Makutano wa  saba (7) wa akimataifa wa jumuiya ya  Mamlaka za usimamizi wa usafiri  Majini Barani Afrika utakaofanyika kuanzia tarehe  29 novemba  hadi 10 Disemba 2024 jijini Dar es salaam. Akizungumza na waandishi wa habari Waziri  wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amesema lengo la mkutano  huo ni kujadili  masuala muhimu  ya maendeleao ya udhibiti na usimamizi wa usalama wa usafiri majini hatani afrika. Amesema  kipaumbele kikiwa ni mustakabali wa usafiri wa majini ma kuongeza ushirikiano baina ya nchi na wanachama. "Kauli mbiu ya mkutano huo ni ' Kuimarisha mustakabali wa sekta ya usafiri majini barani Afrika, ushirikianao katika teknolojia na ubunifu  ili kupunguza hewa ukaa, kuimarisha  usalama wa mazingira,  na  mazingira  ya sekta ...

TAMASHA LA FILAMU BEIJING AFRICAN LAZINDULIWA DAR

Image
Na Brigitte Davis Msimu wa Matangazo ya Tamthiliya na Filamu za Televisheni za Beijing Afrika umefunguliwa rasmi   Dar es Salaam, ukiongozwa na Idara ya Televisheni na Redio ya Beijing.  Tamasha hilo linaadhimisha miaka 10 ya ushirikiano thabiti kati ya Beijing na nchi za Afrika kupitia maonyesho ya filamu bora, likiimarisha urafiki na mawasiliano ya kiutamaduni kati ya China na Afrika. Sherehe za uzinduzi zimefanyika Dar es Salaam na kuhudhuriwana viongozi kutoka Idara ya Televisheni na Redio ya Beijing, Bodi ya Uendelezaji wa Filamu ya Tanzania, Baraza la Sanaa la Tanzania (Basata) na wadau mbalimbali wa sekta ya filamu kutoka pande zote mbili. Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Televisheni na Redio ya Beijing, Dong Dianyi, amesema kuwa tamasha hili limekuwa daraja muhimu la mawasiliano ya kiutamaduni kati ya China na Afrika.  “Miaka kumi iliyopita, tamasha hili lilianza barani Afrika, na sasa limekuwa alama ya urafiki wa kweli kati ya watu wa pande hizi mbili. Tunatazam...

NICE TO MEET YOU IMEZINDULIWA RASMI KUONESHWA SWAHILI PLUS

Image
Na Brigitte Davis TAMTHILIA ya 'Nice to Meet you' inayowakutanisha waigizaji  Lulu Abas 'Lulu Diva' na Hemed Suleiman 'Hemed 'PHD' waliokuwa na uhasama imezinduliwa rasmi na kuwafanya wao kumaliza tofauti zao. Wawili hao inasemekana walianza tofauti zao tangu walipokuwa lokesheni wakirekodi Tamthilia hiyo iliyowahusisha na ugomvi wao kuendelea hadi kwenye maisha yao ya kawaida. Lakini wawili hao wameombana msamaha na kuendelea na maisha yao baada ya kumaliza tofauti zao hizo. Akizungumza na waandishi wa habari Hemed PHD alisema kuwa yeye ndio aliyebeba thamthilia hiyo ya 'Nice to meet you' itakayo kuwa inarushwa Startimes kupitia chanel ya Swahili Plus. "Ushiriki wangu katika tamthilia hii Mimi  ndio muhusika Mkuu na nimeigiza kama mtumishi wa Mungu nimeigiza humo ndo unatakiwa kumfatilia kuanzia uzinduzi rasmi hadi tamthilia yenyewe Watanzania wajiandae kumuona Saimon Mlokole. "Natoa shukrani zangu kwa wote tulioshirikiana ni tamthilia yen...

OVAH YANAPINGA MANENO YA UDHALILISHAJI

Image
Na Brigitte Davis TAASISI ya Ovah Tanzania imesema inapinga maneno ya udhalilishaji yanayotolewa kwa wanawake kwenye maeneo ya wazi ya kijamii kwa kuwa kuyachukulia kawaida  kunamfanya mwanamke  ajihisi hayuko salama. Hayo yamesemwa Dar es Salaam juzi na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Modesta Joseph kwenye uzinduzi wa mradi wa Jamii Salama Initiative (JSI) utakaotumika kutoa elimu dhidi ya maneno ya udhalilishaji kwa wanawake, program itakayofanywa kwa ushirikiano na taasisi nyingine mbalimbali. Modesta alisema baadhi ya maneno wanayoitwa wanawake kwenye maeneo ya Masoko, kwenye vituo vya mabasi a mitaani yakiwemo Chura, Paka na mengine yanayoashiria udhalilishaji yanapaswa kukemewa na kila mmoja kwa usalama wao. "Ni maneno machafu ambayo yamekuwa yakiwafanya wanawake wengi hawana amani, tumekuja na mradi wa JSI ili tuendelee kutoa elimu kwa madereva, masokoni na maeneo mengine ya wazi umuhimu wa kuheshimiana na kulindana ili kutengeneza jamii salama,"alisema. Alisema pia, w...

DRAMAAND MOVIE BROADCAST SEASON IN AFRICA

Image
Beijing TV Dramas&Movies Broadcasting Season in Africa--Celebrating a Decade of Cultural Exchange, Ushering in a New ChapterContent:In September 2024, the Forum on China-Africa Cooperation in Beijing reaffirmed the commitment to deepen ties between China and African nations, working towards a shared future.  Media continues to play a pivotal role in this collaboration, serving as a bridge for cultural exchange and information-sharing.  On November 18, the “Beijing TV Dramas&Movies Broadcasting Season in Africa” will launch, bringing a fresh wave of acclaimed shows under the “Beijing Audiovisual” brand to African audiences, promoting greater understanding between Chinese and African peoples. A Decade of Stories Bringing China and Africa TogetherSince its inception in 2014, the “Beijing TV Dramas&Movies Broadcasting Season in Africa” has introduced high-quality Chinese TV shows to over 30 African countries in languages including English, French, Portuguese, and Swahi...

AAT NGAZI USALAMA ELIMU BARABARANI KWA WANAFUNZI NI MUHIMU

Image
Naibu Kamishna wa Polisi Kamanda Kikosi Maalumu Usalama barabarani Kamanda DCP Ramadhani Ngazi amesema suala la elimu ya  usalama barabarani kwa wanafunzi ni muhimu kuwapa ili kupunguza ajali zisababishwazo na uzembe wa madereva. Amesema elimu kwa Wanafunzi  ni jambo linalohitaji kuunganisha nguvu za pamoja ili kuokoa kundi hilo  kwa bahati mbaya wao  ni miongoni mwa watumia na wako hatarini   zaidi wanapovuka barabra za maeneo ya shulea na majumbani . Akizungumza na wanafunzi na walimu katika shule saba za Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, wakati akifunga mafunzo ya Tathmini za shule zilizopatiwa elimu hiyo  Naibu Kamishna wa Polisi Kamanda Kikosi Maalumu Usalama barabarani Ramadhani Ngazi  amesema kuwa Wametoa mafunzo ya mwezi mmoja katika shule 11 zilizopo katika Wilaya ya Ilala na Kinondoni. "Mafunzo waliyopatiwa baadhi ya waalimu na wanafunzi yanakwenda kuwa chachu kubwa kwa wengine  kupunguza ajali za barabarani husasani kwa w...

MKUTANO MKUU WA TEF KUFANYA KESHO

Image
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) wametangaza kufanya Mkutano  Mkuu wa  Mwaka  unatarajia kufanyika kesho Novemba 7 mwaka huu katika ukumbi wa NSSF uliopo Ilala jijini Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Deodatus Balile amesema kuwa Mkutano huo wa nane utahudhuliwa na zaidi ya wanachama 168 ambao tayari wamethibitisha kushiriki katika Mkutano huo. "Mkutano mkuu 8 utafunguliwa kesho na Mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Habari  Teknolojia, Mawasiliano na habari Jerry Silaa, kwa mara ya kwanza tangu awe Waziri wa Wizara hiyo atakutana na kuongea na waandishi na Wahariri. "Tutakuwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Robert Chalamila na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mpogolo wote wamethibitisha kuwepo na kujadili pamoja nasi. "Katika Mkutano huu tunatarajia kujadili na kuingiza wanachama wapya zaidi ya 20 wenye vigezo na masharti ambapo mwanachama anatakiwa kuwa na cheti cha diploma na uzoefu wa kutosha katika Tasnia ya habari."amesema Balile Pia am...

MSIMU WA SITA HELLO! MR RIGHT DKT KUMBUKA NDANI

Image
Shindano la Hello Mr Right! msimu wa sita limezinduliwa rasmi vijana wakihimizwa kutumia nafasi ya kufuatilia kujifunza namna ya kupata wenza sahihi wa maisha yao. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Godfrey Lugalabam 'Gara B' amesema kuwa msimu huu umekuja kitofauti kwa kuongeza watu wapya wa kutoa mafunzo huku  Kaulimbiu yao ikiwa ni  'Usione so' "Lengo ni kuwakutanisha watu wanaotafuta wenza na kuwaunganisha pamoja waweze kutimiza malengo yao ya kujenga familia ya pamoja."amesema Gala B Kwa upande wake mtangazaji wa kipindi cha Hello! Mr Right Aliya Mohammed amesema kuwa Shindano hilo huchukua wadada 12 ambapo watatafuta wenza wao ambao kwao ni Mr Right! mmoja. "Watu wasichukulie Hello! Mr Right kama Shindano la kiuni hapana Shindano hili lina maadili yote na ndio sababu tunawakutanisha kisha  kuwapa ushirikiano katika kutimiza kiapo cha ndoa."amesema Swalehe Nasoro 'Dokta Kumbuka' amesema kuwa atakuwepo kwaajili ya kuw...

LG MOSQUITO AWAY KUFUKUZA MBU

Image
Imebainishwa kuwa uwepo wa teknolojia mpya ya kufukuza mbu Kwa njia ya kiyoyozi itasaidia Kwa kiwango Kikubwa kidhibiti ugonjwa huo ambao umekuwa ni changamoto Kwa nchi zinazoendelea Tanzania ikiwemo. Serikali inaendelea na Mipango yake ya kupanga mikakati ya namna ya kupambana na ugonjwa wa Malaria na Mbu wanaoeneza Ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na  kuhakikisha inaweka mfumo mzuri wa namna ya kupambana na malaria ili kuweza kuokoa nguvu kazi ya Taifa na rasilimali zitakazotumika katika kutibu ugongwa huo. Kauli hiyo imetolewa na Prof Amos Mwakigonja katika katika uzinduzi wa AC yenye teknolojia mpya ya kufukuza mbu Kwa njia ya kiyoyozi iliyobuniwa na kampuni ya LG ambayo inatajwa kuwa na ufanisi mkubwa na rafiki kwa mazingira. Teknolojia hiyo ya kufukuza mbu Kwa njia ya kiyoyozi itawasaidia wa Tanzania kutokung’atwa na mbu na hivyo Kasi ya  watu kupata malaria itapungua na magonjwa yanayoenezwa na mbu pia yatapungua kwa kiasi kikubwa. Aidha Serikali na wadau wanaendelea kuweka ...