TAMASHA LA HIP HOP ASILI KUFANYIKA PWANI
Msanii wa muziki wa HipHop Asili Festival kwa kushirikiana na ubalozi wa Ufaransa umeaanda tamasha la kimataifa la Hip Hop asili lenye lengo la kukuza utamaduni na ushirikiano likionyesha uridhi wa kipekee wa sanaa
Tamasha hilo litafanyika Mkoani Pwani Bagamoyo katika Chuo cha sanaa cha TASUBA ambapo kutakuwa na muunganiko wa talanta za kitaifa na kimataifa katika utamaduni wa HiP HoP
Hayo ameyasema Ofisa Matei Babis Mkurugenzi wa Hip Hop Asili jana usiku kwenye Mkutano na waandishi wa habari ulifanyika Jijini Dar es salaam
Matei Amebainisha kwa kusema kutakuwa na asili band ambapo wanamuziki na wasanii wa kughani mashairi wameshirikiana kuunda mchanganyiko wa pekee wa hiphop lakini pia kutakuwa na upigaji midundo kwa mdomo yaani ( Beatbox)
Ameongezea kuwa mbali na hayo kutakuwa na kutambulishwa kwa (Breaking )kama mchezo wa Olimpiki pamoja na maonyesho ya sanaa ya machata (Graffiti) ambapk kuta za TASUBA zitapendezeshwa kwa usanifu wa graffiti kutoka kwa Wachata Tanzania na Kactus kutoka Ufaransa.
Nae Ofisa utamaduni na michezo ubalozi wa ufaransa Ettenne Pellausy amesema wameunga mkono tamasha hilo ili kukuza na kusapoti utamaduni wa sanaa husasani kwa wanawake
Nae Msanii wa Hip Hop nchini Tanzania Ibrahim Ayoub maarufu Country Wizzy atakakuwa kwenye tamasha hilo amesema mziki huo wa Hip Hop umeonekana hauna nguvu lakini kupitia tamasha hilo litakuza mziki huo na kuwapa thamani wasanii kwenye Stage kubwa
Tamasha hilo ni la nne kufanyika na lilianza mwaka 2021 ambapo miongoni mwa wasanii watakaokuwa kwenye tamasha hilo ni Maalim Nash, Country Wizzy,Machalii watundu,Sinaubi Zawose na Casey kutoka Ufaransa.

Comments
Post a Comment