ALEX MSAMA AWAASA VIJANA KUHESHIMU NA KULINDA MALI ZA NCHI
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Ndugu Alex Msama amewaasa Vijana na Watanzania wote kwa ujumla kuheshimu na kulinda mali za nchi kwa ajili ya kizazi kiliopo na kijacho, hii ni baada ya baadhi ya vijana usiku wa jana kufanya uharibifu wa miundombinu ya Magari yaendayo kasi maarufu kama Mwendokasi.
Msama amesema Serikali inatumia kodi ambazo zinakusanywa kutoka kwa Wananchi na kufanya maendeleo hivyo si vyema kutoka na kuenda kuharibu miundombinu hiyo.

Comments
Post a Comment